Penina Malundo na
Maua Mashu
Wafanyakazi wakiwemo vibarua zaidi ya 200
wa Kampuni ya STRABAG inayojenga barabara ya mabasi yaendayo kasi jijini Dar es
Salaam wamegoma.
Mgomo huo ulianza jana jijini humo kwa madai ya kutaka kulipwa
stahiki zao za zamani kabla ya kampuni hiyo kuingia mkataba na kampuni
nyingine.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana na waandishi wa
habari, wafanyakazi wa kampuni hiyo walisema kuwa, wameingia katika kampuni
hiyo kwa sheria zote na wengi wao wameweza kufanya kazi zaidi ya mwaka mmoja,
hivyo wanapaswa kulipwa madai yao kabla ya kuvunja mkataba na Kampuni ya
STRABAG.
Walisema kuwa, mgogoro mkubwa uliibuka kati ya vibarua hao
na kampuni iliyoingia mkataba na Strabag ijulikanayo kama
Laba Constractors juu ya malipo watakayolipwa kuwa madogo tofauti na malipo ya
Kampuni ya Strabag.
"Jumamosi tulikaa kikao na viongozi wa Laba
Constractors wakatueleza kuwa kuanzia siku ya Jumatatu (juzi), malipo yetu
yatakuwa chini yao, kwani wameingia mkataba na Kampuni ya Strabag kwa ajili ya
kulipa wafanyakazi wake na vibarua, jambo la kushangaza sisi hatujapata taarifa
yoyote kutoka kwa Strabag juu ya mkataba huo walioingia na Kampuni ya Laba
Constractors," alisema mmoja wa vibarua hao ambaye hakutaka kutaja jina lake.
Alisema kuwa, Kampuni ya Strabag ingefanya utaratibu
maalumu wa kumaliza madai yote ya msingi kwa vibarua wake na hapo ndipo
wangeweza kuanza kuingia mkataba na kampuni nyingine.
"Mpaka sasa hatujui hatma yetu, sisi tumekaa hapa toka
saa 12 asubuhi na tutaendelea kukaa mpaka kieleweke hadi tupatiwe haki yetu,
malipo yetu tupewe ndiyo kampuni nyingine ianze upya na sisi, kwani tumeshakaa
zaidi ya mwaka mmoja, kisheria sisi tayari ni wafanyakazi halali,"
alisema.
Naye Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi katika Kampuni ya
STRABAG (TAMICO), Abdullah Rukusa alisema kuwa, Kampuni ya Strabag ilikuwa
inawalipa vibarua hao malipo ya sh. 12,500 kwa siku huku malipo ya posho yakiwa
sh. 4,800 kwa saa za ziada.
Alisema kuwa, Kampuni ya Laba Contractors inataka kuwalipa
vibarua hao kiasi cha sh.10,000 kwa siku hali itakayofanya kampuni hiyo
kuwanyonya wafanyakazi hao pindi wanapoanza kazi saa 12 asubuhi hadi saa 12
jioni.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Laba
Contractors, Emanuel Mshana alisema kuwa, mkataba kati yao na Kampuni ya Strabag ulisainiwa Jumamosi
iliyopita na kazi rasmi ilianza kufanyika juzi huku tayari akidai wamekutana na
wafanyakazi hao kwa mazungumzo.
Alisema kuwa, vibarua 95 waliopewa na Kampuni ya Strabag
kati yao 45 ndio walioanza kufanya kazi nao juzi
na kampuni yao
kuongeza vibarua 28 kwa siku, kwa ajili ya kufanya kazi.
Juhudi za kumtafuta Mkurugenzi wa Kampuni ya
Strabag ziligonga mwamba baada ya kugoma kuzungumza na waandishi wa habari huku
geti likizuiliwa na mawe makubwa ya barabaran
No comments:
Post a Comment