Frank Monyo na Daniel Samson
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali
za Mitaa (TAMISEMI), Zuberi Samatabe, amewahimiza walimu wa shule za msingi
kuwajengea wanafunzi utamaduni wa kujisomea vitabu ili kuongeza uelewa katika
masomo yao.
Aliyasema hayo
katika uzinduzi wa tovuti ya kufuatilia mgawo wa vitabu vya chenji ya Rada
uliofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Lengo la
tovuti hiyo ya www. pesptz.org ni kutoa taarifa kwa wadau wa elimu pamoja na
wanafunzi juu ya vitabu vinavyosambazwa katika shule za msingi kwa kutumia
chenji hiyo.
Alisema,
Serikali ya Uingereza iliamuru fedha zilizotumika vibaya katika manunuzi ya
Rada zirudishwe kwa Watanzania na zitumike katika manunuzi ya vitabu na
madawati kwa shule za msingi.
"Fedha za
chenji ya Rada sh. bilioni 72 zilizorudishwa ziliingizwa katika mpango wa
manunuzi ya vitabu na madawati katika shule za msingi na asilimia 75 zimetumika
katika manunuzi ya vitabu vya wanafunzi na vya mwongozo wa walimu
kufundishia," alisema Samatabe.
Kwa upande wake Meneja Takwimu wa Kampuni ya
Data vision International, William Kihula alisema Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI
kupitia Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Uingereza (DFID) iliwapa jukumu la
kutengeneza tovuti kufuatilia mgao wa vitabu vya chenji ya Rada, ili kuwezesha
ushirikishwaji wa wadau wa elimu na wananchi katika kufuatilia usambazaji wa
vitabu shuleni.
Alisema hatua hii itawezesha serikali
kuendelea kutembelea katika maeneo yake na kuwa na uendeshaji wa uwazi ndio
maana wamejenga mfumo huu katika namna ambayo itaweza kutumika na wizara hata
baada ya mradi huo wa mgawo wa vitabu vya chenji ya rada kuisha.
"Tovuti hiyo
ndio pekee inayoweka mtandaoni majina yote ya shule za hapa nchini wilaya na
mikoa iliyopo hii itatoa mwanga wa kuanzia katika ufuatiliaji wa maendeleo ya
mwanafunzi mmoja mmoja," alisema Kihula.
Aliongeza kuwa, kuwepo kwa jitihada za Wizara
ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kuanza kutumia mfumo mpya wa kupima ufaulu wa
wanafunzi kwa kuhusisha "Continous Assessment" kwa kuanza na shule za
sekondari.
"Katika hili
Datavision tupo kwenye hatua za mwisho za kutengeneza mfumo wa teknolojia
itakayowezesha kupatikana na kutunza taarifa za maendeleo ya mwanafunzi shuleni
kwa wakati," alisema Kihula.
No comments:
Post a Comment