Na Grace Ndossa
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba (NHC),
Nehemia Mchechu ametunukiwa tuzo ya uongozi bora pamoja na cheti kwa kutambua
mchango wake mkubwa katika jamii na ndani ya shirika hilo.
Tuzo hiyo ilikabidhiwa
jana jijini Dar es Salaam
na Rais wa Rotary Klabu ya Mzizima, Ambrose Nshala ambapo alieleza kuwa
Mkurugenzi huyo amekuwa kiongozi bora na amethubutu kufanya kazi kwa ujasiri na
kuonesha ndoto za kufika mbali.
Alisema kuwa, Mkurugenzi
huyo ni kijana mdogo, lakini ameonesha uthubutu wake katika kufanya kazi na
mageuzi ndani ya shirika, hali ambayo imeonesha hatua kubwa kiuchumi na kazi
anazofanya zitalifikisha mbali shirika.
Alisema kuwa, Rotary klabu
inathamini mchango wake na kutambua kazi aliyofanya kwa jamii kwani ni kubwa
hivyo wametoa tuzo hiyo na cheti kwa ajili ya kuongeza hamasa kwa viongozi
wengine kuiga mfano wa mkurugenzi huyo ili nchi iweze kupata maendeleo.
Kwa upande wake, Mchechu
alisema kuwa, tuzo hiyo itasaidia kuongeza hamasa zaidi katika kufanya kazi ili
nchi iweze kupata maendeleo.
Alisema kuwa, sera za Tanzania ni
nzuri ila tatizo liko kwenye utekelezaji kwani viongozi wengi wanathamini
maneno kuliko vitendo, hivyo ndiyo vinavyofanya mambo mengi kukwama.
Pia
alisema, sera nyingi hapa nchini nyingi huishia kwenye karatasi na nchi nyingi
huiga sera za Tanzania
katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ndiyo maana zimepiga hatua
Mimi sidhani anastahiki tuzo yoyote. Kwanza shirika la NHC limejaaa rushwa, ubadhirifu na uzembe. Angalia jengo lililoporomoka na kuua watu 35 hapa jijini. Ingawa NHC ni mbia katika mradi huo yeye amesema hakuwa na habari kuwa jengo hilo liliongezwa magorofa kinyemela na kinyume cha sheria
ReplyDelete