15 November 2013

STEWART HALL APATA ULAJI MWINGINE



Na Mwandishi Wetu
  Kocha aliyeachana na timu ya Azam FC raia wa Uingereza, Stewart Hall amepata ulaji wa kufundisha soka katika Academy mpya ya Symbion Power itakayoanzishwa hivi karibuni.

 Academy hiyo itaanzishwa nchini kwa ushirikiano wa Klabu ya Sunderland AFC ya Uingereza na Wizara ya Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo.
 Kabla ya kuanzishwa mradi huo, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Fenella Mukangara alikwenda nchini Uingereza na kwenda katika Klabu ya Sunderland akiwa na Rais Jakaya Kikwete kufikia makubaliano ya mradi huo.
  Akizungumza Dar es Salaam jana Mtendaji Mkuu wa Symbion Power Tanzania, Peter Gathercole alisema Academy hiyo itakuwa na vituo eneo la Kidongo Chekundu na Elite Football Academy, Dar es Salaam.
  Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Sunderland, Margaret Byne alisema mradi huo utasaidia kuinua soka la vijana, timu za taifa na klabu.
Alisema ili soka liweze kupiga hatua ni lazima lianzie kwa vijana wadogo ambao wanatakiwa kufundishwa mbinu, maarifa na kujengewa uimara.

No comments:

Post a Comment