- NI BAADA YA RAIA WAKE WATATU KUNASWA NA KAGASHEKI
- SASA KUSHIRIKIANA NA TANZANIA KUPAMBANA NA UHALIFU
Hussein
Makame, MAELEZO na Penina Malundo
Serikali ya China
imesema itashirikiana na Tanzania
kufanya uchunguzi wa tuhumu zanazowakabili raia watatu wa nchi hiyo wanaodaiwa
kukamatwa wakiwa na meno ya tembo 706 jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Hayo yalisemwa
na Naibu Mkuu na Mshauri wa Masuala ya Kisiasa wa Ubalozi wa China nchini Tanzania,
Li Xuhang, wakati alipozungumza na waandishi wa habari kwenye ubalozi wa nchi
hiyo, jijini Dar es Salaam.
Alisema Balozi wa China
nchini Dkt. Lu Youqing pamoja na ubalozi wake wanalaani vikali kitendo hicho
cha mauaji ya tembo na magendo ya meno na kwamba nchi hiyo iko tayari
kushirikiana na Tanzania
kupambana na wahalifu.
Aliongeza kuwa Serikali ya China inaunga mkono kwa dhati Serikali ya Tanzania kupingana na magendo ya meno ya tembo
na Jeshi la Polisi la nchi yake linapenda kushirikiana na Jeshi la Polisi la Tanzania
kupambana na wahalifu.
Alifafanua kuwa ubalozi huo umestushwa na
habari hiyo iliyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari nchini na kwamba sasa
upande wa China unafanya
uchunguzi kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania ili kupata uhalisia wa
habari hiyo.
"Jana (juzi) na leo (jana) tumepeleka
maofisa wa Ubalozi wetu ku chunguza kwanza kuthibitisha utambulisho wa watu hao
na pia tumeliambia Jeshi la Polisi kwamba hawa watu watatu kama ni raia wa
China haki zao za msingi lazima zilindwe," alisema Xuhang.
Aliongeza kuwa; "Tumeamua kufanya
uchunguzi wa kina kwa sababu hatuwezi kufanyia kazi taarifa za vyombo vya
habari, hivyo lazima tuthibitishe taarifa hizi na ikiwa ni za kweli tutakuwa tayari
kuisaidia Serikali ya Tanzania
kuwafikisha mahakamani wahusika."
Alifafanua kuwa kufanya magendo ya meno ya
tembo ni kosa kubwa la jinai kwa nchi ya China
na adhabu kali inatolewa kwa mtu anayepatikana na kosa hilo
ikiwemo kama atakutwa na kilo sita za meno
hayo anafungwa jela miaka kumi au zaidi.
"Ikiwa utapatikana na hatia ya meno ya
tembo ya zaidi ya kilo sita unaweza kuhukumiwa jela miaka zaidi ya kumi au
kunyongwa kabisa, kwa hiyo Serikali ya China
inaongoza duniani kwa kutoa adhabu kali kwa kosa hilo," alisema Xuhang.
Aliwataka raia wote wa China wanaoishi Tanzania
kufuata Sheria za China na
za Tanzania na kwamba
wasifanye kitendo chochote kinachokwenda kinyume na sheria kama
vile kufanya magendo ya meno ya tembo
No comments:
Post a Comment