Na Rachel Balama
Mahakama
Kuu, Kanda ya Dar es Salaam, inatarajia kufanyia mapitio ya uamuzi wa kutupilia
mbali ombi la upande wa utetezi la kutaka kufutwa kwa shtaka la kutotii amri
halali ya mahakama linalomkabili Shekhe Ponda Issa Ponda.
Ombi hilo
lilitupiliwa mbali na Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro, Richard
Kabate. Mapitio hayo yanatarajiwa kufanyika Novemba 18, mwaka huu.
Mawakili wa Ponda wakiongozwa na Juma
Nassoro, waliiomba mahakama hiyo kupitia uamuzi huo uliotolewa Oktoba mosi,
mwaka huu na hakimu huyo.
Hakimu Kibate alitupilia mbali ombi la upande
wa utetezi uliokuwa ukiomba mahakama hiyo kuondoa shtaka hilo la kutotii amri halali linalomkabili
mteja wake au lifutwe akidai kuwa ilitolewa na Mahakama ya Kisutu.
Wakili Nassoro alidai kwamba amewasilisha
ombi hilo baada ya kubaini kuwa mahakama hiyo ya
Morogoro haina uwezo kisheria kusikiliza shtaka hilo, vinginevyo lifunguliwe katika Mahakama
ya Hakimu Mkazi Kisutu ambayo ilitoa hukumu hiyo.
Hata hivyo, Hakimu Kibate alitupilia mbali
ombi hilo na kusema kuwa kwa mujibu wa vifungu
mbalimbali vya sheria vya uendeshaji wa kesi za jinai, shtaka hilo dhidi ya Ponda la kudaiwa kutokutii amri
halali ya mahakama litaendelea kusikilizwa katika mahakama hiyo na sio
kuhamishiwa Kisutu.
Alizitaja sababu za shtaka hilo
kuendelea kusikilizwa katika mahakama hiyo kuwa ni mshtakiwa huyo kutenda kosa hilo eneo la Kiwanja cha
Ndege la Manispaa ya Morogoro.
Hakimu huyo alisisitiza kuwa hakuna sababu ya
kuhamishiwa shtaka hilo katika Mahakama ya Kisutu.Sababu nyingine ni mshtakiwa
huyo kuvunja amri halali iliyotolewa na Mahakama ya Kisutu na sio sharti kama
ambavyo upande wa utetezi ulidai na kufafanua kuwa hata kama mahakama hiyo
ilitoa sharti, kisheria sharti linalotolewa na mahakama yoyote ni amri.
Sheekhe Ponda anakabiliwa na
mashtaka matatu anayodaiwa kuyatenda kwenye mhadhara huo. Ilidaiwa mahakamani
kwamba aliwaambia Waislamu wasikubali uundwaji wa kamati za ulinzi na usalama
za misikiti kwani zimeundwa na ambao ni vibaraka wa CCM na serikal
Uonevu tuuu hakuna jpyaaaa..
ReplyDelete