12 November 2013

POLISI: WALIOMPIGA MVUNGI NI HAWA

  • SASA WAFIKIA TISA, WAKUTWA NA MAPANGA,SIMU YAKE





 Rehema Maigala na Isaya Ng wijo
Jeshi la Polisi nchini, linawashikilia watuhumiwa tisa wanaosh ukiwa kumvamia, kumjeruhi na kuiba vitu mbalimbali vya Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu yaC hama cha NCCR-Mageuzi, Dkt.Sengondo Mvungi.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Sa laam jana, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt. Emmanuel Nchimbi,alis ema kukamatwa kwa watuhumiwa hao, kumechangiwa na ushirikiano uliotolewa na familia ya Dkt. Mvungi.
Alisema watuhumiwa hao wamekamatwa jijini Dar es Sa laam kwa nyakati tofauti ambapo awali walikamatwa sita lakini majina yao yalifichwa ili kutovuruga upelelezi.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova,ambaye alikuwepo katika mkutano huo, waliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Msigwa Mpopela (30) ,Shabago Magozi na Hamadi Ally, jina maarufu‘Hatibu’.
Wengine ni Zakaria Raphael (dereva wa bodaboda), Mmanda Saluwa,Juma Hamisi,Longisho Semeriko(muuza ugolo), Paul Jeirosina mwingine aliyemtaja kwa jina moja la Kilimimazoka,am bao wote ni wakazi wa Dar es Salaam.
“Watuhumiwa hawa walikutwa na mapanga, kigoda ambavyo vim ethibitika kuwa vilitumika katika tukio hilo, pia wa likutwa na simu ya m kononi mali ya Dkt. Mvungi,”alisema.
Kamishna Kova alisema, katika mahojiano ya awali na watuhumiwa, walikiri kuhusika na tukio hilo na ushahidi umekamilika kwa asilimia 80.
“Watuhumiwa wote wamekiri kosa hivyo tunakamilisha upelelezi ili wafi kishwe mahakamani mara moja,”alisema .
Dkt. Mvungi alivamiwa, kujeruhiwa na watu wanaodhaniwa kuwa majambazi usiku wa kuamkia Novemba 3 mwaka huu , nyumbani kwake Kibamba, Dar es Salaam.
Hivi sasa,Dkt. Mvungi anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Milpark, nchini Afrika Kusini na hali yake inaendelea kuimarika .
Akizungumzia suala la kuwakamata wahamiaji haramu, Dkt.Nchimbi alisema mpango walionao ni kuweka Ofisa mmoja wa Polisi kila Tarafa nchini aweze kusaidiana na Polisi Jamii pa moja na wananchi kuwabaini watu hao.

1 comment:

  1. Ningependekeza kuwepo na road blocks pembezoni mwa mji zitakazokaliwa na jkt na polisi za kudumu.

    ReplyDelete