12 November 2013

NITAMNG’OA SPIKA MAKINDA-MBUNGE



  •  ASEMA CCM HAIWEZI KUONDOA HOJA YAKE BUNGENI
  • ASISITIZA MSIMAMO WAKE KWA WAPIGA KURA JIMBONI

Na Suleiman Abeid, Nzega
   Mbunge wa Nzega mkoani Tabora ,Dkt.Hamisi Kig wangalla,amesema bado ana dhamira ya kuwasilisha hoja ya kumng’ oa madarakani Spika  wa B unge, Bi.Anne Makinda .Alisema uvumi ulioenea kuwa hoja yake imeondolewa kwa agizo la Chama Cha Mapinduzi (CCM), hauna ukweli
.  Dkt. Kigwangalla aliyasema hayo mwishoni mwa wiki katika mkutano wa hadhara ulioshirikisha wakazi wa jimbo hilo na vitongoji vyake uliofanyika katika Uwanja wa Parking.Katika mkutano huo, Dkt. Kigwangalla aliulizwa swali na mkazi wa jimbo hilo kama kweli ana ubavu wa kumng’oa Bi.Makinda, anayetokana na chama chake.
“Mheshimiwa mbunge,naomba utu thibitishie kama una uwezo wa kumng’oa Spika wa Bunge (Makinda), kama ulivyotangaza dhamira ya kuwasilisha hoja binafsi bungeni ili bunge liweze kumng’oa.
“Kwa jinsit unavyofahamu utaratibu ndani ya CCM, huna ubavu wa kufanya hivyo , inaonesha ulikuwa ukijifurahisha tu,”alihoji mwananchi huyo.
Mwananchi huyo aliongeza kuwa, kwa kawaida CCM ina utaratibu wa kuzuia hatua mbalimbali zinazotaka kuchukuliwa na wanachama wake hivyo alimshauri Dkt.Kigwangalla, aacha ne na hoja hiyo kwani hana ubavu wa kumng’oa Bi.Makinda.
Akijibu swali hilo,Dkt. Kigwangalla alisema,si kweli kwamba CCM ina utaratibu wa kuondoa kinyemela hoja ambazo haikubaliani nazo ambapo suala la kutaka kumng’oa Bi. Makinda lipo ndani ya uwezo wake na kufafanua kuwa, hoja hiyo haijaondo lewa na hivi sasa ipo katika hatua za mwisho ili iweze kufikish wa bungeni.
“Kwa hili la kumng’oa Spika wa Bunge,niwaeleze wazi kuwa si kweli linawezaku nishinda... hoja imewasilishwa na Bi.Makin da atang’oka kama nikiamua kuendelea nayo kwa sababu tayari hoja nimeiwasilisha na nimekidhi mashart iyote.
“Hivi tunavyoongea, hoja yangu tayari imetoka hatua ya kwanz a na kukidhi vigezo vyote sasa inaenda hatua y a pili ambayo Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge,itaamua ho ja yangu iingizwe bungeni au isiingizwe,”alisema .
Aliongeza kuwa, baada ya hapo utafuata mcha kato wa mwisho ambao ni hoja hiyo kufikishwa bungeni na yeye kuiwasilisha rasmi mbele ya Bunge ili kufanyiwa uamuzi na wabunge wote kwa kupiga kura na kama atashinda au kushindwa,hilo ni jambo lingine.
Dkt.Kigwangalla alisema uamuzi wa kuondoka au kutoondoka kwa Spika, kutategemea uamuzi wa wabunge wenzake na kusisitiza kuwa , CCM haiwezi kuzuia hoja hiyo bila ya kupatiwa uamuzi na wabunge wote.
Akijibu swali ambalo lilihusiana na fedha za ushuru wa huduma zilizotolewa na Mgodi wa Dhahabu wa Resolute, ulioko wilayani humo, Dkt. Kigwangalla alisema fedha hizo sh. Bilioni 2.340,zililipwa na mgodi huo na sasa zimehifadhiwa katika ak aunti maalumu ili baadaye zitumike kama mtaji wa kuanzishia Ben ki ya Maendeleo ya Wananchi wa Nzega .
“Fedha hizi tulizipigania kwa kiasi kikubwa hadi kuandam ana lakini tulifanikiwa kuzipata, niwathibitishie zipo sa lama katika akaunti maalumu tuliyoianzisha ili baadaye ziweze kuanzisha Benki yetu ya Maendeleo ambayo itaweza kutupa mikopo ya kuendesha shughuli zetu,”a lisema .
Alisema lengo lake ni kuhakikisha fedha hizo zinatumika vizuri ili kuwasaidia wananchi wa Nzega kubadilisha maisha yao ambapo watu watahamasishwa kujiunga katika ushirikaau SACCOS ili waweze kupewa mikopo pia zitatumika kununulia mitambo ya kutengeneza barabara na uchimbaji visima vya maji.
Gazeti moja linalotoka kila siku (si Majira), liliandika habari inayosema Dkt. Kigwangalla anadai Bi. Makinda amekiuka kanuni kwa kuidhinisha malipo ya sh. 430,000 kama posho kwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, tofauti na wajumbe wa kamati nyingine ambao malipo yao ni sh. 180,000 kwa siku.
Hoja hiyo ilipingwa vikali na baadhi ya wabunge akiwemo Mbunge wa Tabora Mjini, Bw. Ismail Aden Rage (CCM) na Mbunge wa Kigoma Kusini, Bw. David Kafulila (NCCR-Mageuzi) ambao walidai hawaoni sababu ya kumuondoa Bi. Makinda madarakani.
Bw. Kafulila alisema hilo ni suala la wana-CCM, kwani Bi. Makinda aking’olewa madarakani, mtu ambaye ataziba pengo lake hawezi kutoka upinzani. Hoja hiyo ya Dkt. Kigwangalla iliibua mjadala kwa baadhi ya wabunge na wengine kukataa kusaini karatasi ambayo walipelekewa ili kuunga mkono.
Mbunge wa Ludewa, mkoani Njombe, Bw. Deo Filikunjombe, alisema hoja ya Dkt. Kigwangalla imejengwa katika msingi hafifu isiyozingatia masilahi mapana ya nchi na mtazamo finyu

No comments:

Post a Comment