- ASEMA CCM HAIWEZI KUONDOA HOJA YAKE BUNGENI
- ASISITIZA MSIMAMO WAKE KWA WAPIGA KURA JIMBONI
Na
Suleiman Abeid, Nzega
Mbunge wa Nzega
mkoani Tabora ,Dkt.Hamisi Kig wangalla,amesema bado ana dhamira ya kuwasilisha
hoja ya kumng’ oa madarakani Spika wa B
unge, Bi.Anne Makinda .Alisema uvumi ulioenea kuwa hoja yake imeondolewa kwa agizo
la Chama Cha Mapinduzi (CCM), hauna ukweli
. Dkt. Kigwangalla aliyasema hayo mwishoni mwa wiki katika
mkutano wa hadhara ulioshirikisha wakazi wa jimbo hilo na vitongoji vyake uliofanyika katika
Uwanja wa Parking.Katika mkutano huo, Dkt. Kigwangalla aliulizwa swali na mkazi
wa jimbo hilo kama
kweli ana ubavu wa kumng’oa Bi.Makinda, anayetokana na chama chake.
“Mheshimiwa mbunge,naomba utu thibitishie kama una uwezo wa
kumng’oa Spika wa Bunge (Makinda), kama ulivyotangaza
dhamira ya kuwasilisha hoja binafsi bungeni ili bunge liweze kumng’oa.
“Kwa jinsit unavyofahamu utaratibu ndani ya CCM, huna ubavu
wa kufanya hivyo , inaonesha ulikuwa ukijifurahisha tu,”alihoji mwananchi huyo.
Mwananchi huyo aliongeza kuwa, kwa kawaida CCM ina
utaratibu wa kuzuia hatua mbalimbali zinazotaka kuchukuliwa na wanachama wake
hivyo alimshauri Dkt.Kigwangalla, aacha ne na hoja hiyo kwani hana ubavu wa kumng’oa
Bi.Makinda.
Akijibu swali hilo,Dkt.
Kigwangalla alisema,si kweli kwamba CCM ina utaratibu wa kuondoa kinyemela hoja
ambazo haikubaliani nazo ambapo suala la kutaka kumng’oa Bi. Makinda lipo ndani
ya uwezo wake na kufafanua kuwa, hoja hiyo haijaondo lewa na hivi sasa ipo
katika hatua za mwisho ili iweze kufikish wa bungeni.
“Kwa hili la kumng’oa Spika wa Bunge,niwaeleze wazi kuwa si
kweli linawezaku nishinda... hoja imewasilishwa na Bi.Makin da atang’oka kama nikiamua
kuendelea nayo kwa sababu tayari hoja nimeiwasilisha na nimekidhi mashart iyote.
“Hivi tunavyoongea, hoja yangu tayari imetoka hatua ya
kwanz a na kukidhi vigezo vyote sasa inaenda hatua y a pili ambayo Kamati ya Bunge
ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge,itaamua ho ja yangu iingizwe bungeni au isiingizwe,”alisema
.
Aliongeza kuwa, baada ya hapo utafuata mcha kato wa mwisho ambao
ni hoja hiyo kufikishwa bungeni na yeye kuiwasilisha rasmi mbele ya Bunge ili kufanyiwa
uamuzi na wabunge wote kwa kupiga kura na kama atashinda au kushindwa,hilo ni jambo
lingine.
Dkt.Kigwangalla alisema uamuzi wa kuondoka au kutoondoka kwa Spika,
kutategemea uamuzi wa wabunge wenzake na kusisitiza kuwa , CCM haiwezi kuzuia hoja
hiyo bila ya kupatiwa uamuzi na wabunge wote.
Akijibu swali ambalo lilihusiana na fedha za ushuru wa huduma zilizotolewa
na Mgodi wa Dhahabu wa Resolute, ulioko wilayani humo, Dkt. Kigwangalla alisema
fedha hizo sh. Bilioni 2.340,zililipwa na mgodi huo na sasa zimehifadhiwa
katika ak aunti maalumu ili baadaye zitumike kama mtaji wa kuanzishia Ben ki ya
Maendeleo ya Wananchi wa Nzega .
“Fedha hizi tulizipigania kwa kiasi kikubwa hadi kuandam ana lakini
tulifanikiwa kuzipata, niwathibitishie zipo sa lama katika akaunti maalumu
tuliyoianzisha ili baadaye ziweze kuanzisha Benki yetu ya Maendeleo ambayo itaweza
kutupa mikopo ya kuendesha shughuli zetu,”a lisema .
Alisema lengo lake ni kuhakikisha fedha hizo zinatumika vizuri ili
kuwasaidia wananchi wa Nzega kubadilisha maisha yao ambapo watu watahamasishwa kujiunga
katika ushirikaau SACCOS ili waweze kupewa mikopo pia zitatumika kununulia
mitambo ya kutengeneza barabara na uchimbaji visima vya maji.
Gazeti moja linalotoka kila siku (si Majira), liliandika habari
inayosema Dkt. Kigwangalla anadai Bi. Makinda amekiuka kanuni kwa kuidhinisha
malipo ya sh. 430,000 kama posho kwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Bajeti,
tofauti na wajumbe wa kamati nyingine ambao malipo yao ni sh. 180,000 kwa siku.
Hoja hiyo ilipingwa vikali na baadhi ya wabunge akiwemo Mbunge wa
Tabora Mjini, Bw. Ismail Aden Rage (CCM) na Mbunge wa Kigoma Kusini, Bw. David
Kafulila (NCCR-Mageuzi) ambao walidai hawaoni sababu ya kumuondoa Bi. Makinda
madarakani.
Bw. Kafulila alisema hilo
ni suala la wana-CCM, kwani Bi. Makinda aking’olewa madarakani, mtu ambaye
ataziba pengo lake
hawezi kutoka upinzani.
Hoja hiyo ya Dkt. Kigwangalla iliibua mjadala kwa baadhi ya wabunge na wengine
kukataa kusaini karatasi ambayo walipelekewa ili kuunga mkono.
Mbunge wa Ludewa,
mkoani Njombe, Bw. Deo Filikunjombe, alisema hoja ya Dkt. Kigwangalla imejengwa
katika msingi hafifu isiyozingatia masilahi mapana ya nchi na mtazamo finyu
No comments:
Post a Comment