Na Mwandishi Wetu
Rais Jakaya Kikwete,
amemtumia salamu za rambirambi Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),
Philip Mangula, kufuatia kifo cha mtoto wake, Peter Philip Mangula,
kilichotokea juzi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) alikokuwa
amepelekwa kwa matibabu akisumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu.
"Nimeshtushwa, nimesikitishwa na kuhuzunishwa sana kutokana na taarifa
za kifo cha mwanao (Peter Philip Mangula)," alisema kwa masikitiko Rais
Kikwete katika salamu zake.
Rais Kikwete aliongeza kusema kuwa; nasikitishwa zaidi na
taarifa za kifo hiki kwa kuzingatia kwamba ni katika kipindi kifupi
kilichopita, Mangula alimpoteza binti yake, Neema Nemela Mangula aliyefariki
dunia kutokana na ajali ya gari, hivyo ni dhahiri kwamba kifo cha kijana wake
huyu kimeongeza machungu na simanzi kwa familia ya Mangula na kimesababisha
pengo kubwa kwa wanafamilia kwa ujumla.
"Kutokana na taarifa hizo za kusikitisha, ninakutumia
wewe salamu zangu za rambirambi na pole nyingi kwako wewe binafsi na kwa
familia yako yote kwa ujumla kwa kupotelewa na mtoto wako."
Alisema
anamuomba Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema mjalie yeye na familia yake moyo wa
uvumilivu na ujasiri ili kuhimili machungu ya kuondokewa na kijana wao.
Can considering that this neural performs enable experts develop a more desirable personal computer? https://imgur.com/a/AXLLPbn https://imgur.com/a/FQZYnbd https://imgur.com/a/5s067L2 https://imgur.com/a/Q8LzDdD https://imgur.com/a/3ougTMW https://imgur.com/a/ZrdVWG3 https://imgur.com/a/bblaAls
ReplyDelete