Na
Elizabeth Joseph, Dodoma
Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimepanga kuiburuza mahakamani Mamlaka
ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) kwa kosa la kubomoa nyumba za wananchi bila
fidia.
Uamuzi huo ulitolewa juzi na Mkurugenzi wa Organizesheni na Mafunzo
Taifa (CHADEMA), Benson Kigaila wakati akihutubia wananchi katika mikutano wa
hadhara uliyofanywa katika Kata ya Mkonze na Kikuyu Kusini mkoani humo ambapo
alisema kuwa hivi karibuni wakazi wa maeneo hayo walitangaziwa kubomolewa
nyumba zao na CDA kwa madai kuwa wameyavamia.
Kigaila aliwataka wananchi wanaoishi katika maeneo hayo kujiorodhesha
majina yao ili
kupitia chama hicho waweze kutafuta wakili kwa ajili ya kuweka pingamizi la
kusitisha ubomoaji huo.
Kigaila alisema kuwa CDA ilitakiwa kufanya kazi ya kustawisha mji na
kuondoka lakini cha kushangaza hadi leo bado iko Dodoma
na kuwanyanyasa wananchi kwa kuwauzia viwanja kwa bei ya kiasi kisichopungua
milioni 5 pindi wanapohitaji viwanja na wakati mwingine kufukuzwa katika ardhi
ambazo wamezikuta toka enzi za mababu zao jambo ambalo ni kuwanyima haki ya
kumiliki ardhi yao.
Hivyo ili kutetea haki ya wananchi chama
hicho kimeona ni vyema kuungana na wananchi katika kuishtaki Mamlaka hiyo ili
kujua suluhu ya wakazi wa mkoa huu .
Aliongeza kuwa hata chama kilichopo
madarakani (CCM) kimekuwa kikifumbia macho kero za wananchi wa mkoa huu
kuhusiana na Mamlaka hiyo kwani taarifa juu ya CDA inajulikana lakini kimekuwa
kikipiga danadana katika kutoa uamuzi wa kuiondoa mamlaka hiyo ili wazawa
waweze kujua suluhisho la maisha yao
katika kumiliki ardhi ambayo walifukuzwa bila kulipwa fidia.
Aidha, aliwataka wananchi kwa pamoja kupinga
suala la CDA kuvunja maeneo yao bila fidia na kuungana na chama hicho katika
kutetea haki yao ili waweze kuishi kwa amani katika ardhi ya nchi yao pamoja na
kuwataka wananchi kuondoa ukereketwa wa vyama ili kufanikisha suala hilo.
Mkazi mmoja aliyejitambulisha kwa jina la
Mussa Ndalu katika Kata ya Mkonze alisema kuwa Chama kilichopo madarakani ndio
kinaoongoza kwa kuwagawanya Watanzania kwa kuyafumbia macho malalamiko ya
wananchi juu ya umiliki wa ardhi ya nchi yao
huku wageni wakipewa kipaumbele katika suala hilo.
No comments:
Post a Comment