Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert
Manumba, amestaafu rasmi kazi kwa mujibu wa sheria baada ya kufikisha
umriwamiaka 60.Katika utumishi wake ndani
ya Jeshi la Polisi, amefanya kazi katika nyadhifa mbalimbali zikiwemo chumba
cha kupokea mashtaka kuanzia mwaka (1976-1977).
Nafasi nyingine ni
Mwendesha Mashtaka Wilaya ya Kibondo na Kasulu, mkoani Kigoma (1977- 1984),
Mkufunzi wa Chuo cha Polisi Dar es Salaam,
(1984-1987), Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Magomeni, Kinondoni na Naibu Mkuu wa
Upelelezi Mkoa wa Dar es Salaam
(1987-1993),
Taarifa iliyotolewa Dar es Salaam jana na Msemaji wa jeshi hilo, SSP Advera Senso, ilisema Manumba pia
aliwahi kuwa Mkuu wa Upelelezi mkoani Arusha (1993- 1995), Mkufunzi Mkuu wa Chuo
cha Polisi Moshi (1995-1996) na Mkuu wa Kitengo cha Fraud Makao Makuu ya
Upelelezi (1996-1997).
Nafasi nyingine Mkuu wa
Kitengo cha Usalama wa Nchi, Intelijensia na Dawa ya Kulevya Makao Makuu ya
Upelelezi (1997- 2001) na Msaidizi wa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya
Jinai nchini (2001-2006).
Alisema kuanzia 2006 hadi
anastaafu, alikuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (DCI).Mkuu
wa jeshi hilo nchini, IGP Said Mwema,
amemshukuru Manumba kwa kulitumikia Taifa katika nyadhifa mbalimbali ndani ya
jeshi hilo kwa
weledi na uaminifu mkubwa wakati wote wa utumishi wake.
Alimtaka aendelee kuwa
msaada kwa jeshi hilo, kutoa ushirikiano wa
namna yoyote unaoweza kupunguza uhalifu nchini kwa sababu suala la usalama ni
taaluma kama zilivyo taaluma zingine na
taaluma hiyo wanayo watu wachache.
SSP
Senso alisema, wakati taratibu za uteuzi wa DCI mpya zikiendelea, Mkuu wa
Ufuatiliaji na Tathmini CID Makao Makuu, Kamishna Isaya Mungulu, atakua
akikaimu nafasi hiyo.
No comments:
Post a Comment