13 November 2013

AIRTEL YATOA VITABU SHULENI



 Na Mwandishi Wetu
  Kampuni ya Simu za Mkononi ya Airtel Tanzania imeamua kupambana na changamoto zinazoikabili sekta ya elimu nchini kwa kuzisaidia shule mbalimbali za sekondari kupata miundombinu ya kufundishia na vifaa vya kujifunzia.

  Pia kampuni hiyo kupitia mradi wake wa Shule Yetu imewanufaisha wanafunzi wa Shule ya Sekondari Chalinze iliyopo mkoani Pwani baada ya kukabidhi vitabu vya masomo ya sayansi vyenye thamani ya sh. milioni tano kwa shule hiyo.
  Akizungumza wakati wa kukabidhi vitabu hivyo, Meneja Masoko wa Airtel Kanda ya Kusini na Mkoa wa Morogoro, Aminata Keita alisema vitabu hivyo vitatumika katika kuongeza kiwango cha uelewa na kukuza ufaulu kwa wanafunzi wa shule hiyo ambao walikuwa na tatizo la uhaba wa vitabu.
  "Vitabu hivi...vitatumika kukuza ufaulu kwa wanafunzi maana wanafunzi wataweza kujisomea kwa urahisi na kufuatilia masomo kwa ukaribu zaidi," alisema Aminata.
  Aliongeza kuwa, msaada huo wa vitabu ni sehemu ya mpango mkakati wa kuzisaidia shule za kata zinazolalamikiwa kufanya vibaya katika mitihani yao ya kitaifa.
  "Tumetoa vitabu vya masomo ya sayansi tukijua kabisa wanafunzi wengi hushindwa masomo hayo kwa sababu mbalimbali, ikiwemo upungufu wa zana za kujifunzia ila nina imani mradi huu wa Shule Yetu utaziwezesha shule za kata kufanya vizuri kwenye mitihani ya kitaifa," alisema Aminata.
  Kwa upande wake mkuu wa shule hiyo, Emmanuel Kahabi alisema, upatikanaji wa vitabu utarahisisha kazi ya ufundishaji kwa wanafunzi na pia wanafunzi wataweza kuelewa kiurahisi maana zana za kufundishia zinapatikana

No comments:

Post a Comment