Na
Neema Ndugulile
Baraza la Wazee wa Yanga, wameendelea kuvutana na
uongozi wa klabu hiyo kwamba wao wanatambulika kikatiba tofauti na viongozi hao
kuwapinga.Akizungumza na waandishi wa
habari Dar es Salaam jana, Katibu wa baraza hilo, Ibrahim Akilimali alisema
hakuna shina lisilokuwa na mzizi na wao kama wazee ni mzizi wa timu ya Yanga.
Akilimali alisema kwa sasa
Yanga ndiyo imeanza Ligi Kuu upya na wao kama mzizi wa klabu hiyo,
watahakikisha timu yao
inaendelea kusonga mbele.
"Sisi kama wazee wa Klabu ya Yanga, tumesimama
kuhakikisha tunasonga mbele bila kusuasua, sisi ndio mizizi wa klabu na hakuna
shina lisilokuwa na mizizi na hata kama
tukiondoka sisi watakuja wazee wengine," alisema.
Aliongeza kuwa wao kama
wazee, hawajajitenga na hawawezi kujitenga kwani wana umuhimu mkubwa katika
kutoa ushauri, ili kuikuza klabu hiyo
No comments:
Post a Comment