Na Ibrahim Mussa
Redd’s Miss Tanzania,
Happiness Watimanywa jana alitembelea rasmi Kampuni ya Bia Tanzania (TBL),
ambao ni wadhamini wa Mashindano hayo, ambapo alikutana na uongozi wa juu ili
kujitambulisha.
Katika ziara hiyo, Happiness alifuatana na mshindi
wa pili, Latifa Mohammed, mshindi wa tatu, Clara Bayo pamoja na Kamati ya
Redd's Miss Tanzania.
Akizungumza mara baada ya kukutana na mrembo
huyo, Mkurugenzi Mkuu wa TBL, Robin Goestache alisema, wao kama wadhamini wakuu
wanajisifu kuwa sehemu ya mafanikio ya Redd's Miss Tanzania, huku akimsifu mrembo huyo
kwa ushindi wake.
"Kila mmoja kati yetu anajua shindano
lilivyokuwa gumu, warembo wote walikuwa na sifa na ninawapongeza ninyi
mlioshinda na tunawakaribisha katika familia ya TBL," alisema.
Mkurugenzi
wa Masoko wa TBL, Kushillah Thomas, naye alitumia fursa hiyo kuwapongeza
warembo hao na kusema ana imani kubwa nao; watafanya vizuri zaidi katika
kipindi chao, kwa upande wake Meneja Masoko wa TBL, Fimbo Butallah alisema,
tangu waanze kudhamini shindano hilo wamepata mafanikio makubwa mno, huku
kukiwa na kazi nyingi za jamii wanazozifanya na warembo waliofanikiwa kutwaa
taji hilo.
Happiness naye aliishukuru TBL kwa kudhamini
shindano hilo
na kusema anajivunia kwa kiasi kikubwa kuwa sehemu ya familia ya Redd's. "Kwa
kiasi kikubwa nawashukuru kutokana na kudhamini shindano hili kwa muda wa miaka
13, kwani mmewasaidia mengi warembo; na najivunia kuvaa sura ya Redd's,"
alisema.
No comments:
Post a Comment