Na Yusuph Mussa, Lushoto
Walimu watano kwenye Halmashauri
ya Bumbuli wilayani Lushoto mkoani Tanga wanalipwa mishahara wakiwa wametoroka
eneo la kazi, huku wengine wakienda kusoma bila kumuaga muajiri wao
Akizungumza kwenye Baraza
la Madiwani juzi Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo,Patricia
Mbigili aliwataja walimu hao watoro kuwa ni William Kilapilo, Wilbert Mbwambo,
Juma Vumba, Ali Mwehuti, Abeli Mkope na Ramadhan Mwande.
"Kilapilo ametoroka tangu 2011, Mbwambo
2012 na Vumba 2012, hawa wote wanafundisha Shule ya Msingi Kwemkomole. Wengine
ni Mwehuti 2012 na Mkope 2012 Shule ya Msingi Kwamhe na Mwande wa Shule ya
Msingi Kwediwa ametoroka mwaka 2011.
"Walimu hawa wametoroka eneo la kazi na
kwenda kusoma bila utaratibu, lakini tutazingatia maazimio yenu madiwani kuwa
tusimamishe mishahara ya walimu hao mara moja," alisema Mbigili ambaye pia
ni Ofisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Bumbuli.
Diwani wa Kata ya Milingano, Ramadhan Hozza ambaye ni mmoja wa
walioathirika kwa kutorokwa na walimu alisema elimu ya Tanzania inashuka kwa mambo mengi kwa vile
baadhi ya walimu wanatumia ngazi ya kuajiriwa kama
sehemu ya wao kwenda kusoma, lakini si kufundisha watoto wao.
Diwani wa Kata ya Vuga alisema, baadhi ya
walimu hawakai kwenye vijiji vyenye shule wanazofundisha, bali mjini, matokeo
yake inabidi wapangiwe ratiba ya kuanza kufundisha saa nne kwa vile wanafika
wakiwa wamechelewa..
TANGU HIYO 2011 MLIKUWA WAPI?
ReplyDelete