23 October 2013

SERENGETI BOYS YAALIKWA OLIMPIKI



 Na Fatuma Rashid
  Timu ya taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Serengeti Boys), imealikwa kushiriki Olimpiki ya Afrika itakayofanyika Mei mwakani.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Boniface Wambura alisema soka ni kati ya michezo 22 itakayoshindaniwa katika mashindano hayo , yatakayofanyika Gaborone, Botswana chini ya Kamati za Olimpiki za Afrika (ANOCA).
  Wambura alisema kwa mujibu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Tanzania imepewa nafasi ya kushiriki katika michezo hiyo ya Olimpiki kwa Afrika, kutokana na kuwa na programu nzuri za vijana hasa chini ya umri wa miaka 17.Alisema hiyo itakuwa ni michezo ya pili ya Afrika kwa Olimpiki, ambapo ya kwanza ilifanyika mwaka 2010 jijini Rabat, Morocco.

No comments:

Post a Comment