10 October 2013

NGUVU ZA CHADEMA ZAMTISHA MANGULA


Na Mariam Mziwanda
  Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania (Bara), Philip Mangula ameshangazwa na chama hicho kuwa na ‘jeshi’ kubwa la wanachama, lakini linazidiwa nguvu na jeshi dogo la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), hatua ambayo imemfanya aamke na kusoma alama za nyakati kwa kuwarudia wananchi.

Akizungumza na Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Dar es Salaam pamoja na waandishi wa habari jana kabla ya kuanza ziara yake jijini, Mangula alisema;
“CCM ina jeshi kubwa la wanachama lakini linashindwa na jeshi dogo la CHADEMA ambalo halina hata anuani... hivyo nimeona ipo haja kurudi kwenu kuanzia ngazi ya chini kupitia matawi, shina na wananchi mnieleze tatizo ni nini?”
Alisema ili kufikia wananchi nkoani Dar es Salaam, atafanya ziara katika wilaya zote za mkoa huo na kukutana na watendaji, wanachama na wananchi kwani kila mwana CCM ni askari wa mstari wa mbele, lakini anashangazwa na nguvu ndogo iliyopo sasa.
“Chama kikiwa na nguvu ndipo na Serikali inavyokuwa na nguvu, umefika wakati tuelewe kuwa ni muhimu chama kiwasemee watu na si viongozi wa chama wakisemee; hivyo uhai wa chama ni jambo muhimu kwa wana CCM,” alisema
Alieleza kuwa makundi yaliyotokana na uchaguzi wa 2010 ndani ya chama hicho, bado yapo na yanaendelea kwa kasi, hali iliyoathiri zaidi Chama mpaka kufikia mwaka 2012, hivyo mkakati wa kujua vipi yaondolewe pasipo kuathiri zaidi 2014 mpaka 2015 unahitaji kuwepo na mipango imara.
Mangula alisema katika ziara yake hiyo ya mafunzo ambayo imetokana na kutambua kuwa nguvu ya chama ni uwepo wa wanachama, atatenga muda mwingi kuzungumzia changamoto zinazowakabili na kuwagawa wana CCM.
  Alisema kwa kufanya hivyo atapata sababu zinazokwamisha maendeleo ya chama hicho. Alihimiza wana CCM kuelewa kuwa katika wiki ya maadhimisho ya kumbukumbu ya Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere, ipo haja kuenzi harakati zake kwa kukiongezea nguvu chama.
Mangula alisema kujenga chama kunahitaji kujitoa hata kufikia kuacha nafasi ya madaraka kama alivyofanya Mwalimu Nyerere.
 “Wakati wa wiki ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere ni muhimu kuwa na chama chenye nguvu na kujitoa kwani Mwalimu aliacha hata nafasi ya Uwaziri Mkuu na k umuachia Mzee Rashid Kawawa kwa lengo la kurudi katika kazi za ujenzi wa chama na pia tukumbuke Mwalimu aliacha kazi ya Urais mwaka 1985 na nafasi yake kuchukuliwa na Rais Mwinyi, ambapo yeye alirudi tena kufanya kazi za chama hivyo kukijenga chama kunahitaji kujitoa ili kiweze kuwa na nguvu kubwa,” alisema  



4 comments:

  1. sasa tangia Mwalimu Nyerere achie madaraka na kujenga chama atuambie mwengine nani alie fanya hivyo.nadhani Bw Mangula sababu ya kuanguka kwa CCM ni ulevi wa madaraka ulioigupika CCM pamoja na UFISADI unaolindwa.

    ReplyDelete
  2. KINACHOTAKIWA NA KILA CHAMA NI KUFANYA CHAGUZI KUANZIA NGAZI YA KATA HADI TAIFA ILI KUPATA UWAKILISHI HALALI NA WA KIDEMOKRASIA KINYUME CHAKE MAKUNDI YA KIHUNI TU NI SAWA NA KUWAPA SERIKALI WAHUNI WA LIBYA NA MISRI MPAKA LEO HAKUNA AMANI WALA UTENGAMANO ILA MATAIFA YA MAGHARIBI WANAFURAHIA KWANI FURSA NZURI YA KUIBA RASILIMSALI ZA AFRIKA NI VEMA KUWACHUNGUZA VIBARAKA WA NDANI KAMA AKINA CHANGIRAI WA ZIMBABWE MBONA KAANGUKIA PUA SIKU ZA MNAFIKI NI CHACHE KILA MBUNGE ATATOA HESABU 2015 NI NANI ALIYEPANDA MBEGU NA NINANI ALIYEPANDA UPEPO

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kutoa hesabu ni kwa wote haijalishi uko tawala ama upinzani. Ueleze umehamasisha vipi maendeleo katika jimbo lako. Sio umahamasisha maandamano na na chuki vipi katika taifa lako

      Delete
  3. hivi bado kunawatu wanatumia kichwa kufugia nywele nili na wapi na nani uliona kafanya maandamiano ya chuki au yasiyo na tija kojoa ukale.

    ReplyDelete