04 October 2013

KIBADENI AIHOFIA RUVU SHOOTING



 Na Neema Ndugulile
  Kocha Mkuu wa Simba, Abdallah Kibadeni amekataa kuwataja majeruhi katika kikosi chake kwa kuhofia kuhujumiwa na timu pinzani, Ruvu Shooting.

  Simba na Ruvu Shooting, zinatarajia kumenyana kesho katika mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara, inayotarajiwa kupigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
  Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Dar es Salaam jana, Kibadeni alisema hawezi kuwataja majeruhi waliopo katika kikosi hicho kwa kuwa akifanya hivyo atawapa nafasi wapinzani wao kujipanga.
  Licha ya kocha huyo kukataa kuwataja majeruhi hao alisema ana taarifa ya Miraji Adam, ambaye aliumia kidole na hajaruhusiwa kufanya mazoezi.   Akizungumzia mechi hiyo ya kesho, Kibadeni alisema itakuwa ngumu hivyo wataingia kwa hadhari ili kutoka na ushindi. "Mchezo huo unahitaji umakini wa hali ya juu na ndiyo maana tumejipanga vyema kukabiliana na Ruvu kwa hali yoyote uwanjani," alisema

No comments:

Post a Comment