NAIROBI, Kenya
Serikali
ya Kenya imeilaumu Serikali ya Marekani kwa kuwaonya raia wake wasisafiri
kwenda nchini humo kutokana na shambulizi la Septemba 21 mwaka huu, katika
jengo la biashara la Westgate, jijini Nairobi, nchini humo.
Waziri wa Mambo ya Ndani nchini Kenya, Bw. Joseph Ole Lenku, alitoa lawama hizo
jana kwa waandishi wa habari wakati akizungumzia uchunguzi wa Serikali juu ya
shambulizi hilo
linalodaiwa kufanywa na wanamgambo wa Al Shabaab.
Bw.
Lenku alisema kuwa, tahadhari hiyo kwa raia wa Marekani si ya kirafiki na Kenya ingawa uchunguzi huo, ulikuwa ukifanywa na
polisi wa nchi hiyo, makachero wa Israel, Marekani na Ulaya.
Alipinga na kulaani ushauri wa Marekani kwa
raia wake na kuwataka wathamini hali ya usalama wao binafsi kutokana na vitisho
vya kigaidi vinavyoendelea na vya hivi karibuni katika Taifa hilo la Afrika Mashariki.
Ingawa hakuitaja moja kwa moja sekta ya
utalii, maelezo ya Bw. Lenku yanaonekana kuhofia biashara hiyo nchini humo
jinsi inavyoweza kuathirika katika kipindi hiki kwani sekta hiyo inaingiza dola
za Marekani bilioni moja kila mwaka.
“Tumesikitishwa na
ushauri huo ambao haukustahili, hauna umuhimu na si urafiki...unapingana na
mapambano dhidi ya ugaidi wa kimataifa,” alisema Bw. Lenku.
Kwa mujibu wa Shirika la Habari
la Reuters la Uingereza, mbali na wahanga 50 wa Kenya, raia kutoka
Uingereza, Ufaransa, China, Ghana, Canada, Australia, Afrika Kusini, Peru na
Uholanzi pia waliuawa katika shambulizi hilo la kigaidi
No comments:
Post a Comment