Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha
Mapinduzi (CCM), Balozi Seif Ali Iddi, amesema kauli aliyoitoa bungeni Mjini
Dodoma hivi karibuni juu ya Zanzibar
kushirikishwa katika mchakato wa Marekebisho ya Mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri
ya Muungano, ilikuwa sahihi, anaripoti Mwajuma Juma, Zanzibar.
Balozi Seif
aliyasema hayo juzi kwa nyakati tofauti wakati akizungumza na Wajumbe wa
Halmashauri Kuu CCM, mikoa ya Kusini na Kaskazini Pemba akiwa katika ziara yake
ya siku mbili kisiwani humo.
Alisema
amelazimika kueleza ukweli huo kutokana na tuhuma zinazotolewa dhidi yake na
kambi ya upinzani kudai amekurupuka kutoa kauli hiyo bungeni na kudai kuwa,
hapungukiwi kwa lolote.
“Acha
waendelee kunitukana na kunikashifu mimi sitopungua, nilichokisema bungeni Dodoma ni sahihi, kuna ushahidi pamoja na kumbukumu zote
zinazothibitisha ushiriki wa Zanzibar
katika suala hili muhimu,” alifafanua Balozi Iddi.
Balozi Iddi
ambaye pia ni Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar,
mamlaka ya kutunga mswada wa sheria ni kazi ya Serikali ambayo hushirikisha
wataalamu na wadau wa sekta zote kazi ambayo inaishia unapowasilishwa katika
Kamati ya Bunge.
Alisema Sheria
ya Bunge la Katiba ilifikishwa Zanzibar,
kujadiliwa na kufanyiwa uchambuzi kupitia wadau wa sekta hiyo waliotoa nyongeza
ya baadhi ya vipengele ambavyo vyote vilikubaliwa na kamati iliyosimamia mswada
huo.
“Sheria ya
Marekebisho ya Mabadiliko ya Katiba imehusisha mambo manne makubwa ambayo ni
kuundwa kwa Kamati ya kukusanya maoni, kutungwa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya,
Bunge la Katiba na kura ya maoni, mambo haya yalikubalika, kuridhiwa na pande
zote za Muungano, ugomvi uko wapi,” alihoji Balozi Iddi.
Akizungumzia
uimarishaji wa CCM, aliwakumbusha viongozi na wanachama wa chama hicho Kisiwa
Pemba, kuhakikisha wanajenga chama kipindi hiki ambacho ni karibu na Uchaguzi
Mkuu 2015.
Aliwataka
viongozi wa chama hicho mikoa, kuhakikisha vijana wanaandikishwa katika daftari
la kudumu la wapigakura kwani bila kufanya hivyo, hawawezi kupata fursa ya
kupiga kura jambo linaloweza kuisababishia CCM mazingira magumu ya ushindi.
Mjumbe wa
Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Mama Asha Suleiman Iddi
aliwahadharisha viongozi na wanachama kuepuka tabia ya kuendeleza makundi ndani
ya chama hicho.
Alisema tabia hiyo ikiachiwa, inaweza kudhoofisha nguvu za chama na
hatimaye kuleta athari katika harakati zake za kujipanga na ushindi wa kishindo
katika Uchaguzi Mkuu 2015
No comments:
Post a Comment