24 October 2013

HAMIS KIIZA AWAPA FARAJA YANGA SC


  • SIMBA SC YABANWA MKWAKWANI
Na Waandishi Wetu
  Mshambuliaji, Hamis Kiiza wa Yanga jana aliwapa faraja mashabiki wa timu hiyo baada ya kuifungia mabao mawili kati ya matatu, katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom dhidi ya Rhino Rangers ya Tabora.

Katika mechi hiyo iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam mashabiki wa Yanga walionekana kupooza hali inayoonesha kukata tamaa kutokana na matokeo ya Jumapili baada ya kutoa sare ya mabao 3-3 dhidi ya wapinzani wao wa jadi Simba.
Yanga ilianza kupata bao dakika ya 12 lililowekwa kimiani na Kiiza, baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa Simon Msuva aliyetia krosi katika lango la Rhino.Katika dakika za mwanzo timu zote zilicheza mchezo wa kuviziana na kuufanya kuwa wa kupooza, huku Yanga wakifanya mashambulizi ya kushtukiza.
Dakika ya 43 Yanga walikosa bao la wazi kupitia kwa Msuva, ambaye alibutua mpira baada ya kupewa nzuri pasi nzuri na Mrisho Ngassa, ambaye jana alicheza kwa juhudi kubwa kuhakikisha timu yake inaondoka na ushindi.Kipindi cha pili kilianza kwa Yanga kuingia na uchu wa kutaka kufunga, ambapo dakika ya 48 nusura, Msuva angeipatia bao timu hiyo lakini shuti lake likaokolewa na mabeki wa Rhino.
Kiiza aliikosesha Yanga bao la wazi, baada ya kubaki na kipa wa Rhino ambaye aliuwahi mpira na kuudaka..Yanga ilikosa bao lingine dakika ya 70 baada ya Ngassa kufanya kazi kubwa na kutoa pasi nzuri kwa Kiiza ambaye alipiga shuti kubwa lililotoka nje ya lango.
Frank Domayo aliipatia Yanga bao la pili dakika ya 73 baada ya kupokea pasi nzuri ya Ngassa, ambaye alikuwa akihaha huku na huku kutafuta mabao.Dakika ya 73 Yanga iliongeza bao la tatu lililowekwa kimiani na Kiiza, baada ya kupewa pande na Ngassa.
  Naye Hamis Miraji anaripoti kutoka Tanga kuwa, Simba jana ilitoka suluhu na Coastal Union katika mechi ya ligi hiyo iliyochezwa Uwanja wa Mkwakwani.Katika mechi hiyo, Hamis Ndemla wa Simba alikosa bao dakika ya 10 baada ya kuachia shuti kali lililotoka nje ya lango la Coastal.
   Dakika 18 wachezaji wa Simba walipigiana pasi safi hadi ndani ya 18 lakini, Hamis Tambwa alishindwa kutumbukiza mpira kimiani, baada ya kuwa katika nafasi nzuri ya kufunga..Coastal Union nayo ilizinduka dakika ya 19 lakini mshambuliaji wake raia wa Uganda, Yayo Lutimba akiwa ndani ya 18 alishindwa kufunga baada ya shuti lake kutoka nje ya lango. Katika mechi nyingine iliyochezwa Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, Prisons ililazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi Kagera Sugar

No comments:

Post a Comment