19 September 2013

YANGA WAMSHTAKI KALIA KWA TENGA...



Na Elizabeth Mayemba
VIONGOZI wa Matawi ya Yanga Mkoa wa Dar es Salaam wamemshtaki Mwenyekiti wa Kamati ya Ligi Kuu, Wales Kalia kwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga kwa madai ya kuitishia klabu hiyo ambayo inapanga kuandamana.

Katika barua yao iliyowasilishwa jana TFF wanachama hao, wamemtaka Kalia ajiuzulu nyadhifa zake zote ndani ya TFF kwa kuwa ameshindwa kusimamia mpira.Barua hiyo iliyosainiwa na Katibu wao Supa Nyamu, inadai kusikitishwa na kitendo cha kiongozi huyo wa Kamati ya Ligi kupandikiza chuki katika klabu yao kupitia katika kituo kimoja cha redio nchini kwamba atapambana na wanaotaka kuandamana Yanga.
Barua hiyo inaeleza kuwa maneno aliyoyasema Kalia, yanaonesha wazi kuwa si kiongozi kwani anapandikiza chuki binafsi na kuegemea upande mwingine wakati yeye hapaswi kuegemea upande wowote.
“Sisi wanachama na wapenzi wa Yanga wakati timu yetu inahujumiwa yeye anashabikia vitendo viovu vya uvunjifu wa amani inavyofanyiwa klabu yetu ya Yanga.“Kalia kwa matamshi yake aliyotoa katika redio ni kuwadhalilisha wana Yanga wote vitendo vinavyofanywa na waamuzi wanaochezesha Ligi Kuu ni ukiukwaji wa sheria 17 za mpira wa miguu,” ilisomeka sehemu hiyo ya barua. 
 Barua hiyo ilieleza kuwa kwa kauli za kiongozi huyo anaidhalilisha Yanga na kuihujumu, hivyo anapaswa kujiuzulu nafasi zake zote zinazompa mamlaka TFF na kuomba vyombo husika, vimchukulie hatua ya kuondolewa kwenye mchakato wa Uchaguzi Mkuu kwa kuwa naye ni mgombea

No comments:

Post a Comment