09 September 2013

WORLD VISION YAKABIDHI MIRADI YA MAENDELEO



Na Derick Milton, Simiyu
SHIRIKA la World Vision Tanzania limekabidhi mradi mkubwa wa maendeleo kwa wananchi wa Kata za Nkoma na Mwalushu wilayani Itilima mkoani Simiyu uliodumu kwa miaka 16 ambao umenufaisha wananchi 49,608.

Mr a d i h u o amb a o umekabidhiwa mwishoni mwa wiki kwa wananchi ukiwa chini ya Halmashauri ya wilaya hiyo ulianzishwa mwaka 1998 ukiwa na lengo la kuongeza ustawi kwa watu maskini hasa ustawi wa watoto ukiwa chini ya shirika hilo kwa ufadhili wa watu wa nchini Newzeland.
Akitoa ufafanuzi juu mafanikio ya mradi huo tangu kuanzishwa kwake hadi kumalizika Mkurugenzi wa Miradi wa World Vision Tanzania, Dkt. Kasilima Yosh alisema kuwa mradi huo ulikuwa na lengo kuu moja kuleta ustawi kwa kila mtoto.
Al i s ema mr a d i wa m a e n d e l e o N k o m a ulianzishwa mwaka 1998 ambapo hadi kufikia mwisho wake umeweza kuleta maendeleo kwa wananchi katika nyanja za kiuchumi, kiafya, kijamii, kiulinzi, pamoja na kimaamuzi na haki zao kwa ujumla.
Alisema katika idadi hiyo ya wananchi walionufaika na mradi huo wanawake ni 13,273, huku wanaume wakiwa 14,335, watoto wakiwa jumla yao 22,956, wa v u l a n a 1 0 , 9 5 5 n a wasichana wakiwa 12,001.
Alisema katika mafanikio ya mradi huo kwa upande wa sekta ya kilimo na uhakika wa chakula shirika hilo limefanikiwa kuunda vikundi 120 vya wakulima wanaotumia njia nbora za kilimo, matumizi ya mbolea, pamoja na uzalishaji wa mazao umeongezeka kwa kiwango kikubwa.
Aliongeza wakulima wanaotumia njia bora za kilimo wameongezeka kutoka asilimia 7 mwaka 1998 hadi kufikia asilimia 47 kwa mwaka huu, ambapo katika sekta ya afya jumla ya wahudumu wa afya 32 wamepewa mafunzo ya kuhudumia jamii katika huduma za afya.
Alibainisha magonjwa ya kuambukiza yanayotokana na maji nayo yamepungua kutoka asilimia 87 hadi kufikia asilimia 24 kwa mwaka huu, ikiwa pamoja na kupungua kwa utapiamlo mkali na wa kati kwa watoto chini ya miaka 5 kutoka 42 miaka 0.6 na ule wa kati kutoka asilimia 25 hadi kufikia 0.
Aidha alisema katika upande wa elimu katika mradi huo shirika limefanikiwa kujenga jumla ya madarasa 55, kwa kushirikiana na Serikali kukarabati madarasa 9, nyumba 2 za walimu, ofisi 16 za walimu nazo zimejengwa na mradi, vitabu 3,850 vimetolewa kwa shule 11, pamoja na kutoa madawati 1,126 kwa shule 11.
Akipokea mradi huo Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Paschal Mabiti ambaye pia alikuwa mgeni rasmi alilipongeza shirika hilo kwa kazi hiyo kubwa ikiwa pamoja na kuwataka viongozi wa halmashauri kuhakikisha mradi unakuwa endelevu pamoja na kutunzwa.

No comments:

Post a Comment