Na Mwandishi Wetu
Watanzania
wametakiwa kuchangamkia fursa za uwekezaji zinazopatikana katika kisiwa cha
Anjouan nchini Comoro ili kukuza na kuendeleza ushirikiano uliopo kwa maslahi
ya kijamii na kiuchumi kati ya pande hizo mbili.
Gavana
wa Anjouan, Anissi Chamsidine,al ielezah ayoalipotembel eaKituo cha Uwe kezaji
Ta nz ania(TIC) janajijini Dar es
Salaam."Tuna
fursa nyingi za uwekezaji katika kisiwa cha Anjouan na tunaamini Watanzania
wako katika nafasi nzuri ya kuzitumia," alisema na kuongeza kuwa
ushirikiano kati ya pande hizo mbili ni wadamu na wa kihistoria.
Alisema
kuna umuhimu wa kuendelea kushirikiana katika eneo la uwekezaji na kutaja
maeneo ambayo yan ahitaji uwekezaji kuwa ni elimu,utalii,nishati na katika
sekta ya afya."Tuna
hospitali kubwa zinajengwa lakini tatizo ni kukosekana kwa wataalamu wa afya
ikiwemo wauguzi na madaktari hivyo tunaomba Watanzania waje kutusaidia katika
eneo hilo,"
alisema.
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa TIC, Juliet Kairuki amesema kuwa ujio wa
Gavana huyo na ujumbe wa wawekezaji utasaidia kufungua fursa za uwekezaji na
ushirikiano mzuri kiuchumi kati ya nchi hizo.
"TIC
na Serikali inathamini ziara ya Gavana na ujumbe wake, uhusiano wetu ni wa siku
nyingi na tungependa kuimarisha," alisema na kuongeza kuwa ziara hiyo
itasaidia kuvutia uwekezaji kutoka katika kisiwa hicho.
No comments:
Post a Comment