26 September 2013

BALOZI WA HISPANIA KUWASHAWISHI WAFANYABIASHARA KUWEKEZA NCHINI



Na Gladness Mboma

  Balozi wa Hispania nchini,Bw.Luis Cuesta amesema kuwa atawashawishi wafanyabias hara wa nchini mwake kuja kushirikiana na Watanzania kuwekeza katika sekta mbalimbali kwa kuwa ina fursa nyingi za kiuchumi.  Bw.Cuesta aliyasema hayo juzi wakati alipomtembelea Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya IPP, Bw.Reginald Mengi,ambapo alisema Tanzania ikitumia vizuri fursa mbalimbali z ilizopo wana nafasi kubwa ya kupiga hatua za kiuchumi.

  Alitaja fursa zilizopo nchini ni sekta ya gesi,utalii, mafuta na bahari na kusisitiza kwamba ikiwa maeneo hayo yataendelezwa yanaweza kusaidia nchi kupiga hatua kubwa.“Hispania ina watu wapatao milioni 43 ambayo inakaribiana idadi ya Watanzania, lakini sisi tumeweza kupiga hatua katika uchumi kutokana na kujikita katika sekta za nishati na utalii,”alisema.

Alisema kuwa Tanzania ina mazingira mazuri ya kibiashara ikiwemo amani,hali ya hewa, rasilimali, upatikanaji wa gesi na fursa nzuri ambayo inaweza kuwanufaisha Watanzania wote.Naye Dkt . Mengi alisema mazingira mazuri ya uwekezaji yatafanikiwa iwapo wawekezaji kutoka Hispania watakaokuja nchini wataungana na Watanzania katika ushirikiano.

“Kamakutakuw anaushirikiano wa dhatika tika sektambalimbali kati ya wawe kezaji wanjenaWatanz anianc hiinaweza kupigahat uaku bwa zakiuchumi.Dkt.Mengi alisema kuwa kunahaj a yaWatanzania kujifu nzamazu ri kutoka kwaHispaniahusu sanna mnailivyopiga hatuakati kasekta ya nishati na utalii.

No comments:

Post a Comment