05 September 2013

WASOMI WATAKA KINGA YA RAIS IONDOLEWE



 Na Lilian Justice, Mvomero
WASOMI wa Chuo Kikuu Mz umb e k i l i c h o p o wilayani Mvomero mkoani Morogoro wamesema kuwa ni vyema Rais akaondolewa kinga ya kushtakiwa pindi anapotuhumiwa kwa makosa ya rushwa, ufisadi na ubadhirifu wa mali ya umma
. Hayo yalibainishwa jana na wanajumuiya hao kwa nyakati wakati wakijadili rasimu ya katiba kwa mwaka 2013 ambapo Mkurugenzi wa masomo ya shahada ya kwanza chuoni hapo, Prof George Shumbusho alisema ni vyema rais akapewa kinga kwa masuala ya kawaida na si masuala ya rushwa, ufisadi na matumizi mabaya ya rasilimali za umma.
A i d h a w a s o m i h a o wamependekeza Katiba Mpya, k u r u h u s u u a n z i s hwa j i wa Mahakama ya Rushwa kama ilivyo kwa Mahakama za Ardhi, biashara na nyingine, ili kutoa nafasi kwa suala hilo kushughulikiwa kwa mapana zaidi tofauti na hivi sasa.
Pia mwanafunzi wa chuo hicho, Ester Safari alisema kitendo cha kuwapeleka watuhumiwa wa rushwa katika mahakama za kawaida, kumesababisha mrundikano wa mashauri mengi kwa waendesha mashtaka na mahakimu.
Aidha walisema kuwa kesi hizo zimeonekana kukosa nafasi ya kutosha badala yake kuonekana ni masuala ya kisiasa zaidi, hivyo kupendekeza rushwa kuwa na mahakama yake itakayokuwa na waendesha mashtaka wake ili kutilia mkazo vita dhidi ya rushwa.
Kwa upande wake Mhadhiri msaidizi Kitivo cha Sheria chuoni hapo, Dkt. Eliuther Mushi pamoja na mambo mengine, amependekeza suala la jukumu la usafi wa mazingira kwa kila mtu iwe ni wajibu wa kikatiba ili kumfanya Mtanzania kuwajibika na usafi katika maeneo yake badala ya kusubiri kazi hiyo kufanywa na halmashauri.
Aidha Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Taaluma, Prof. Josephat Itika, ameshauri suala la uzalendo kupewa kipaumbele kikatiba na suala la kujitegemea likatambulika kikatiba, ili kijana tangu utoto wake ajue suala hilo ni la lazima.
Aidha wachangiaji wengine, Mhadhiri msaidizi wa chuo hicho, Innocent Mgeta, mwanafunzi, Charles Ntwale na mwezeshaji, Benjamini Jonas, wamependekeza katiba ijayo yenye Serikali tatu iwe na Rais mmoja wa muungano na kwa upande wa nchi washirika yaani Zanzibar na Tanganyika kuwe na mawaziri wakuu ili kupunguza gharama zisizokuwa na lazima.
Hata hivyo wamelitaka suala la ardhi na maziwa kuwekwa wazi katika katiba ili yatambulike wazi, tofauti na sasa jambo linapelekea wananchi kushindwa kushirikishwa na kunufaika na rasilimali hizo.

No comments:

Post a Comment