Na Mwandishi
Wetu
Washibiki wawili waliofanikiwa kuingia fainali za mashindano
ya kuimba la Epiq Bongo Star Search (EBSS) kwa njia ya simu watajulikana wiki
hii, baada ya kuwashinda wenzao zaidi ya 3,000 walioshiriki kupitia simu za
mkononi.
Washiriki hao wawili wataungana na wenzao 10, ambao jana walifanikiwa kuingia hatua
hiyo kati ya 15 waliokuwa wamebaki.Mashabiki
wengi wa mashindano hayo wanawasubiria kwa hamu washiriki hao hasa baada
ya mshiriki kwa njia ya simu wa mwaka jana, Menina Atick, kufanya vizuri.Hadi sasa wamebaki washiriki 10 ambao
ni Amina Chibaba, Elizabeth Mwakijambile, Emmanuel Msuya, First Godfrey,
Francis Flavian, Furaha Charles, Furaha Mkwama, Joshua Kahoza, Maina Thadei na
Mandela Nicolus.
Washiriki waliotoka jana ni Fatma Omary
mshiriki kutokea Dar es Salaam, Joseph Kura
mshiriki kutoka Arusha na Catherine Mtange wa Dar es Salaam.Wengine walioaga ni Joseph
Meteka na Kennedy Gedeon ambapo washiriki waliotolewa kwenye 'danger zone 'na
kurudia katika kundi la washiriki wa kawaida ni Furaha Mkwama na Mandela
Nikolas.
No comments:
Post a Comment