05 September 2013

WANANCHI WAZUA BALAA BAGAMOYO



 Na David John
WANANCHI wa Kijiji cha Kidomole, Kitongoji cha Vihagatta Kata ya F u k a y o s i wi l a y a n i Ba g amo y o mk o a n i Pwa n i wamevamia mashamba yaliyopo katika kijiji hicho na kugawana maeneo kwa madai kuwa viongozi wa halmashauri ya mji huo wanayauza kinyemela kwa watu wasiojulikana
.Akizungumzia na Majira mapema wiki hii, Mwenyekiti wa Kamati maalumu ya wananchi hao, Salum Mubalule alisema wamechoshwa na viongozi hao kwani wamekuwa wakishuhudia maeneo hayo yakiuzwa kwa matajiri wenye fedha zao bila wananchi kuhusishwa ikizingatia kuwa maeneo hayo yalitolewa na wananchi kwa ajili ya huduma za kijamii.
“Haya maeneo tuliyatoa sisi wananchi kwa ajili ya kujenga shule, zahanati, soko na mambo mengine kwa ajili ya maendeleo ya wananchi lakini chakushangaza viongozi hawa wanauza kinyemela tena kinyume na taratibu, hivyo tunaamua kugawana hapa,” alisema.
Aliongeza kuwa wamefanya jitihada mbalimbali zikiwa pamoja na kwenda Wilayani kuripoti matukio hayo kwa nyakati tofauti na wakati mwingine kufikia hata makubaliano yakuendeleza maeneo hayo lakini kadri siku zinavyokwenda maeneo yanazidi kuuzwa.
Naye Katibu wa Kamati hiyo, Samweli Kisoma alisema Serikali ya kijiji imeshindwa kuwasikiliza na hata walivyokwenda wilayani pia wameshindwa kuwajibika hivyo maamuzi yao ni kugawana mashamba hayo kila mwanakijiji achukuwe kilicho chake.
Akijibu tuhuma hizo za wananchi wake Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Ramadhani Mohamed alisema utaratibu wanaoutumia wananchi hao haukubaliki na wanapaswa kuchukuliwa hatua kali za kinidhamu.
Alisema mambo wanayoyaleta kijijini hapo ni ya kisiasa hivyo Serikali ya kijiji itawachukulia hatua wote wanaofanya vurugu hizo ikiwa pamoja na kushawishi watu wengine kwani wanajulikana.
“Mnajua wanaofanya mambo haya wanajulikana na mimi kama mwenyekiti sitakubali vurugu hizi na tutahakikisha tunawachukulia hatua kali wananchi hawa ambao wanahatarisha amani ya kijiji chetu,” alisema.
Aliongeza kuwa kuna kundi la watu ambalo linaongozwa na mwenyekiti ambaye aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Serikali ya kijiji hiki na alitolewa na wananchi hao hao kwa tuhuma mbalimbali na hata mambo hayo ya kuuzwa kwa ardhi yeye alihusishwa huko nyuma.
“Nadhani anachofanya hapa ni kuhamasisha wananchi kufanya vurugu hizi, sasa lazima wachukuliwe hatua kali za kinidhamu ili kukomesha vitendo hivi vya utovu wa nidhamu,” alisema.Naye Mkuu wa Wilaya hiyo, Ahmed Kiponzi aliagiza kukamatwa kwa wananchi hao nakuongeza wanachokifanya hakikubaliki katika nchi inayoongozwa kidemokrasia

No comments:

Post a Comment