02 September 2013

USAILI WAGOMBEA TFF, BODI YA LIGI WAKAMILIKA



Na Mosi Mrisho
USAILI wa waombaji uteuzi kwenye uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Bodi ya Ligi Kuu (TPL Board), ulitarajia kukamilika jana.Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa shirikisho hilo, Boniface Wambura, Kamati ya Uchaguzi ya TFF chini ya Mwenyekiti wake Hamidu Mbwezeleni ilianza usaili juzi ambapo matokeo ya usaili yanatarajiwa kutangazwa kesho.

Alisema kati ya Septemba 4 na 6 mwaka huu, Kamati ya Uchaguzi kupitia Sekretarieti ya TFF itawasilisha kwenye Kamati ya Maadili ya TFF mashauri yote ya maadili, ili kujadiliwa na kutolewa uamuzi na kamati hiyo."Vilevile kati ya Septemba 4 na 6 mwaka huu ni kipindi cha kukata rufaa kwenye Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi kwa masuala yasiyo ya maadili," alisema Wambura.Alisema kwa watakaokata rufaa wanatakiwa kuambatanisha na ada ya rufaa kwa Katibu Mkuu wa TFF, kabla ya saa 10 jioni ya Septemba 6 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment