02 September 2013

MANCHESTER UNITED YALALA KWA LIVERPOOL



 LIVERPOOL, Uingereza
MANCHESTER United jana ilichezea kichapo cha bao 1-0 dhidi ya Liverpool katika mechi ya Ligi Kuu England iliyochezwa kwenye Uwanja wa Anfield mjini Liverpool.Mechi ilianza kwa Man United kulifikia lango la Liverpool lakini mabeki wa Liverpool walisimama imara kuondoa mashambulizi hayo.

Liverpool ilipata bao lake dakika ya nne kipindi cha kwanza lililowekwa kimiani kwa kichwa na Daniel Sturridge akimalizia mpira wa krosi kutoka winga wa kulia.Dakika ya sita nusura Robin Van Persie aipatie Man United bao kwa tiktak, lakini shuti lake lilipaa juu ya goli.
Dakika ya tisa Man United waligongeana pasi vizuri lakini shuti la Danny Wellbeck lilidakwa kiustadi na kipa wa Liverpool.Kipindi cha pili Man United waliingiwa na uchu wa kupata mabao, ambapo dakika ya 46, 49 na 53 ilipata kona tatu mfululizo ambazo, hata hivyo, hazikuzaa matunda.
Dakika ya 71 Nemenja Vidic nusura angeizawadia bao Liverpool baada ya kurudisha mpira fyongo kwa kipa wake David Degea ambao uliwahiwa na mshambuliaji Coutinho ambaye hata hivyo alishindwa kufunga.Licha ya washambuliaji wa Man United Luis Nani, Wellbeck, Chicharito, Ashley Young na Valencia kuwa na uchu wa mabao lakini kikwazo kikubwa kilikuwa kwa kipa wa Liverpo

No comments:

Post a Comment