22 September 2013

SHAMBULIO LAUA WATU 22 NCHINI KENYA



 NAIROBI, Kenya

  Watu 22 wanahofiwa kufariki baada ya watu wenye silaha kufyatua risasi mjini Nairobi, Kenya, kwenye eneo la maduka katika mtaa wa Westlands.Walioshuhudia tukio hilo, wanasema kuwa maguruneti pia yalitumika katika shambulio hilo.


  Kwa mujibu wa Mwandishi wa BBC mjini Nairobi washambuliaji inaarifiwa walivaa vilemba kama vya al-Shabaab, lakini haikuthibitishwa kama wapiganaji hao wamehusika. Taarifa za awali za BBC zilieleza kuwa watu sita waliuawa kwenye shambulio hilo.

  Polisi waliokuwa na silaha walizingira jengo la maduka liitwalo Westgate, katika mtaa wa Westlands na kuna taarifa ya watu waliojeruhiwa walikuwa wakitolewa hapo kwa machela.Ilielezwa kuwa watu wengi walikuwa wamenasa ndani ya jengo.
  Magari yaliyoegeshwa nje ya maduka yaliharibika. Shirika la Habari la Reuters liliarifu kuwa mpiga picha mmoja aliona watu wamelala chini.Hadi sasa hakuna taarifa rasmi kama kuna watu waliokamatwa kwa kuhusishwa na tukio hilo

1 comment: