22 September 2013

MAGEUZI YA KILIMO YAMPAISHA KIKWETE



 Na Mwandishi Maalum
Rais Jakaya Kikwete, ametunukiwa Shahada ya Uzamivu (PhD) ya Udaktari wa Sheria na Chuo Kikuu cha Guelph cha Toronto, Canada, kutokana na mchango wake mkubwa wa kuleta mageuzi ya kilimo nchini na Afrika kwa ujumla
. Rais Kikwete alitunukiwa shahada hiyo juzi katika sherehe ya kufana iliyohudhuriwa na mamia ya wasomi wa chuo hicho wakiwemo wanafunzi na wahadhiri na Wana-jumuya ya Watanzania waishio Canada.  
Rais Kikwete ameitunuku Shahada hiyo kwa niaba ya wananchi wote wa Tanzania na hasa wakulima wadogo ambao wanapigana kufa kupona kuboresha maisha yao kupitia kilimo. Hiyo ni heshima ya juu kabisa ambayo Chuo Kikuu kinaweza kutoa; na Rais Kikwete anakuwa Mtanzania wa kwanza kutunukiwa Shahada hiyo katika historia ya zaidi ya miaka 100 ya Chuo hicho, maarufu kwa utafiti wa kilimo na magonjwa ya wanyama.
Makamu Mkuu wa chuo hicho na Kaimu Rais wa chuo hicho, Dkt. Maureen Mancuso, alifungua rasmi Baraza la Kutunuku Shahada. 
Akieleza sababu ya kumtunuku shahada hiyo Rais Kikwete, Profesa Dkt. Kevin Hall, alisema chuo hicho kimeamua kutoa Shahada hiyo kwa kutambua mchango wake katika kuendeleza, kuboresha na kuleta mageuzi katika kilimo cha Tanzania na Afrika.
“Tumeshuhudia kwa namna isiyokuwa ya kawaida kabisa jinsi gani Rais Kikwete amekuwa sauti isiyochoka ya kusemea kilimo cha Afrika na kuishawishi dunia katika kusaidia kuleta mageuzi na mapinduzi ya kijani katika Bara hili muhimu sana kwa kukabiliana na changamoto zinazokabili kilimo katika Bara la Afrika,” alisema Dkt. Hall ambaye ni Makamu wa Rais wa Chuo hicho anayesimamia shughuli za utafiti.
Aliongeza kuwa kwa miongo mingi hawajashuhudia kiongozi mmoja wa Afrika akijitokeza kwa namna isiyofichika kabisa kukabiliana na changamoto zinazokabili shughuli inayoajiri watu wengi sana na ambayo ni tegemeo kubwa la maisha ya mamilioni ya watu.
“Rais Kikwete tunakushukuru kwa mchango wako mkubwa katika kuleta mapinduzi ya kilimo katika Afrika kupitia progamu zako kama vile Kilimo Kwanza na SACGOT,” alisema.
Rais Kikwete, kama kawaida yake anapozungumzia shughuli za kilimo, ametoa hotuba ya kusisimua ambayo ilizungumzia hali ya kilimo katika Tanzania na Afrika, changamoto kuu za kilimo na hatua ambazo zinachukuliwa kukabiliana na hali hiyo.
   Akizungumzia umuhimu wa kilimo katika Tanzania, alisema kuwa asilimia 75 ya Watanzania wanaishi maeneo ya mashambani na kutegemea kilimo kwa maisha yao na kuwa hata wale wanaoishi mijini uhai wao unategemea kilimo kwa njia nyingi.
 “Kilimo kinatupa chakula tunachokula, mali ghafi ya viwanda vyetu, mapato yetu ya fedha za kigeni na ajira kwa ajili ya watu wetu. Kilimo kinaingiza asilimia 25 ya Pato la Taifa, asilimia 34 ya mapato yetu ya fedha za kigeni, asilimia 95 ya chakula chetu na kinaajiri asilimia 75 ya watu wetu. Kwa ufupi basi, maendeleo ya uchumi na ustawi wetu unategemea kilimo,” alisema.
   Rais alisema pamoja na umuhimu huo wa kilimo kwa Tanzania na Afrika, bado kilimo cha Bara hilo kinabakia cha jadi, kilicho duni na chenye sifa ya uzalishaji mdogo.Niruhusuni nitoe takwimu kufafanua hoja hii. Katika Tanzania hekta moja ya mahindi inazalisha tani 1.3, wastani wa Afrika ni tani 1.9, katika China ni tani 5.7 na hapa Canada naambiwa ni tani 10. Vivyo hivyo, kwa uzalishaji wa mpunga na pamba.
   Akizungumzia umuhimu wa kilimo katika Tanzania, alisema kuwa asilimia 75 ya Watanzania wanaishi maeneo ya mashambani na kutegemea kilimo kwa maisha yao na kuwa hata wale wanaoishi mijini uhai wao unategemea kilimo kwa njia nyingi.
  “Kilimo kinatupa chakula tunachokula, malighafi ya viwanda vyetu, mapato yetu ya fedha za kigeni na ajira kwa ajili ya watu wetu. Kilimo kinaingiza asilimia 25 ya Pato la Taifa, asilimia 34 ya mapato yetu ya fedha za kigeni, asilimia 95 ya chakula chetu na kinaajiri asilimia 75 ya watu wetu. 
   Kwa ufupi basi, maendeleo ya uchumi na ustawi wa wetu unategemea kilimo,” alisema.Rais alisema pamoja na umuhimu huo wa kilimo kwa Tanzania na Afrika, bado kilimo cha Bara hilo kinabakia cha jadi, kilicho duni na chenye sifa ya uzalishaji mdogo.

No comments:

Post a Comment