18 September 2013

SEKONDARI YA ILIBORU YAFUNGWA



Na Pamela Mollel, Arusha
SHULE ya Sekondari Iliboru, iliyopo Wilaya ya Arumeru, mkoani Arusha, imefungwa na Serikali kwa muda usiojulikana baada ya kuwepo kwa hofu ya kuchomwa moto.Chanzo chetu cha habari kilisema kuwa, tangazo la kufungwa shule hiyo lilitolewa jana asubuhi na Mkuu wa shule hiyo, Bw.Julius Shila baada ya kushauriana na Bodi ya Shule hiyo.

Akizungumza na Majira kwa njia ya simu jana, Bw. Shila alikiri shule hiyo kufungwa kwa muda usiojulikana ambapo uamuzi wa kuifungua utatolewa na Ofisi ya Mkoa wa Arusha."Ni kweli shule imefungwa kwa muda usiojulikana kutokana na utovu wa nidhamu ambapo wanafunzi wote wamerejea nyumbani, kuna taratibu ambazo wanapaswa kuzifuata," alisema Bw. Shila.Baada ya tangazo la kufungwa kwa shule hiyo, inadaiwa zaidi ya wanafunzi 800 kuanzia kidato cha kwanza hadi sita, wameathirika wakiwemo wanaofanya mitihani ya mwisho.

No comments:

Post a Comment