Na Mwandishi Wetu, Igunga
WAZIRI Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, amesema
angependa kuona Mkoa wa Tabora unakuwa wa mfano kwa kushirikisha vijana kwenye
kazi za uzalishaji mali.Alisema mkoa
huo umethubutu, umeweza na kinachosubiriwa kwa sasa ni matokeo. Bw. Pinda
aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati akizungumza na viongozi na wananchi wa
Wilaya ya Igunga, mkoani humo
.Kabla ya kuzungumza na viongozi hao, Bw. Pinda alipokea taarifa ya Wilaya katika Kijiji cha Simbo akiwa katika ziara fupi ya kukagua miradi ya uzalishaji inayofanywa na vijana."Mnalolifanya leo si geni, mmetumia ardhi ileile ya Igunga, Mto Manonga na Bwawa la Bulenya vyote vilikuwepo, wakuu wa Wilaya na mikoa walikuwepo, lakini mbona hawakufanya chochote...ninyi mmethubutu," alisema.
.Kabla ya kuzungumza na viongozi hao, Bw. Pinda alipokea taarifa ya Wilaya katika Kijiji cha Simbo akiwa katika ziara fupi ya kukagua miradi ya uzalishaji inayofanywa na vijana."Mnalolifanya leo si geni, mmetumia ardhi ileile ya Igunga, Mto Manonga na Bwawa la Bulenya vyote vilikuwepo, wakuu wa Wilaya na mikoa walikuwepo, lakini mbona hawakufanya chochote...ninyi mmethubutu," alisema.
Aliwataka
viongozi wa Serikali wilayani humo na vyama vya siasa, washirikiane kulea
vikundi hivyo bila kujali wanavikundi wanatoka chama gani na kusisitiza vikundi
husika ni kiungo muhimu cha kuleta maendeleo.
Alisifia mpango
wa kuanzisha kijiji cha vijana katika Wilaya ya Sikonge ambacho alikiita
"Maisha plus", kwa jinsi walivyoamua kuanza maisha katika hali ya
chini wakiwa wamedhamiria kujikomboa kiuchumi kupitia kazi za uzalishaji kama
kilimo, ususi, uchongaji, ufugaji mifugo na nyuki.
Mapema akiwasilisha taarifa ya
maendeleo ya Wilaya hiyo, Mkuu wa Wilaya, Bw. Elibariki Kingu, alisema
wametenga maeneo matano yenye ukubwa wa zaidi ya hekta 250 kwa ajili ya
shughuli za wajasiriamali zinazofanywa na vikundi vya vijana.
Aliitaja miradi hiyo kuwa ni ya kilimo
cha umwagiliaji cha alizeti, mahindi, vitunguu, matikiti maji na mboga za
majani. Miradi mingine ni kutengeneza vyombo vya nyumbani kama vile makarai,
majiko na ndoo kwa kutumia vyuma chakavu pamoja na kusafirisha abiria kwa
pikipiki.
Alisema Wilaya hiyo imeweka mpango
mkakati wa kutumia fursa zilizopo kujenga mazingira ya upatikanaji ajira kwa
vijana kupitia sekta ya kilimo baada ya kubaini kuwa, kilimo cha vitunguu kina
tija kubwa kwani hakihitaji matunzo makubwa kama dawa na pembejeo nyingine.
"Zao hili halilimwi kwa wingi hapa
wilayani kwa sababu watu wengi hawana ufahamu wa matokeo, pamoja na wilaya hii
kuwa kame, ina udongo wenye rutuba nyingi, kuna mabwawa mawili na malambo 51
ambayo pamoja na mahitaji mengine ya maji kwa matumizi ya nyumbani na mifugo,
yanaweza kusaidia katika kilimo cha vitunguu na mbogamboga," alisema.
Akizungumzia upatikanaji wa masoko, Bw.
Kingu alisema bei ya vitunguu imekuwa juu wakati wote bila kujali msimu na kuna
wakati inafika sh. 100,000 kwa gunia moja."Soko la vitunguu lipo kila wakati
ndani na nje ya nchi, wafanyabiashara kutoka nchi jirani za Rwanda, Burundi,
Uganda, Sudan Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), wamekuwa
wakinunua zao hili kutoka Tanzania.
"Wiki ijayo tutakwenda Kenya
kukutana na wafanyabiashara kutoka Sudan na Kenya wanaohitaji vitunguu kwa
wingi." alisema.Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,
Vijana, Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante ole Gabriel Laizer, alisema
mwaka huu wa fedha, Serikali imetenga sh. bilioni sita zikiwa ni fedha za Mfuko
wa Maendeleo ya Vijana.
Alisema idadi ya vijana nchini hivi
sasa imefikia 16,195,370 ambao wanapaswa kubadilisha mtazamo wa fikra zao na
kujitambua kuwa wanaweza kuboresha maisha yao kwa kubainisha fursa zilizopo
kwenye maeneo wanayoishi na kuangalia watazitumiaje badala ya kusubiri kazi za
kuajiriwa ambazo hazipo.
Alisema ameanza mazungumzo na wenzake
walioko Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
ili kupata uhakika wa fedha za vijana kutoka kwenye halmashauri.
No comments:
Post a Comment