Na Suleiman Abeid,
Simiyu
MBUNGE wa Maswa Magharibi, mkoani S imi
y u , Bw. J o h n Shibuda (CHADEMA), amewataka Watanzania kuhakikisha Katiba
Mpya nayo inatambua masilahi, maendeleo yao na kuzingatia misingi ya utawala
bora badala ya kuwanufaisha wanasiasa wenye malengo binafsi
.Bw. Shibuda
aliyasema hayo juzi wakati akiwahutubia wananchi kwenye kilele cha maadhimisho
ya siku ya makumbusho ya mila za Kisukuma yaliyofanyika katika Mji wa Malampaka,
wilayani humo.
Alisema
wananchi wanapaswa kutambua kuwa, katiba ya nchi yoyote duniani ndiyo wokovu wa
uhuru, maendeleo hai ya jamii husika na Taifa ambapo kama Watanzania watazembea
na kusababisha kupatikana kwa katiba mbovu, watakuwa wamejiwekea tanuri la
kukaushia haki zao.
Aliongeza kuwa,
ni muhimu wakawa watulivu, kusoma taswira na mazingira ya kila hatua juu ya
msukumo wa maoni yanayotolewa na makundi mbalimbali kuhusu katiba ijayo iwe na
mfumo gani.
"Tupatapo mawazo ya rasimu toleo
la pili, tuhakikishe tunatafakari na kusemezana kwa madhumuni ya kupata katiba
bora itakayobeba masilahi ya wananchi, tuhakikishe tunapata Katiba Mpya ambayo
itaendeleza umoja wetu wa kitaifa.
"Katiba ijayo ing'arishe
palipotokea uchakavu wa masilahi ya jamii na Taifa, Katiba Mpya iwe nguzo kuu
ya kusimamia ustawi na maendeleo ya uongozi wa kidemokrasia inayotoa fursa za
utawala bora dhidi ya dhuluma kwa jamii," alisema.
Bw. Shibuda alisema katiba
inayohitajika kwa Watanzania iwe mlango wa dira ya kujengwa maisha bora ya
wafugaji, wakulima, wavuvi, watumishi wa sekta ya umma, binafsi na kuiwezesha
nchi kupata viongozi bora.
"Tuwe makini ili tusipate katiba ambayo ni malighafi ya maisha bora
kwa nchi za Ulaya na Watanzania kugeuzwa vibarua na watumwa wa utandawazi
kupitia rasilimali zetu," alisema
No comments:
Post a Comment