- MAHAKAMA KUU YAWAHUKUMU KUNYONGWA HADI KUFA
Na Moses Mabula, Nzega
Mahakama Kuu Kanda ya Tabora imewahukumu
watu watatu kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya kumuua kwa
makusudi mkazi wa Kijiji cha Mbagwa wilayani Nzega mkoani Tabora,Mganga Mgisha,
ili mmoja wa wauaji hao apate fursa ya kuoa mke wa marehemu huyo.
Katika kesi
hiyo, mmoja wa wauaji hao, Kulwa Makomelo alikuwa na njama za kutaka kumuoa mke
wa marehemu huyo,Catherine John, ambapo ilidaiwa alimlipa kiasi cha sh. 20,000
muuaji mwenzake, Kisena Lutonja, ili amsaidie kufanikisha mauaji hayo.
Mke wa marehemu
huyo ni miongoni mwa waliohukumiwa adhabu hiyo. Akitoa hukumu hiyo iliyochukua
muda wa saa tatu, Jaji Amiri Mluma, alisema mahakama imeridhika na ushahidi
uliotolewa kuwa washtakiwa hao walipanga mauaji hayo.
Alisema washtakiwa
wamepatikana na shtaka hilo
la kupanga kuua na kufanya mauaji."Walipanga makusudi kumuua Mugisa, hivyo
mahakama inawahukumu kunyongwa hadi kufa ili iwe fundisho kwa watu wengine.
Jaji huyu aliiambia mahakama hiyo
kwamba; "Kutokana na kukithiri kwa vitendo vya watu kushambuliana kwa
mapanga bila sababu na kujichukulia sheria mkononi natoa adhabu hii ili iwe
fundisho kwa watu wa aina hiyo."
Awali, mwanasheria wa Serikali,
Iddforce Makandara, aliiambia mahakama hiyo kuwa watuhumiwa hao wote kwa pamoja
walimuua, Mugisa kwa kumpiga kitu kizito kichwani na kisha kumshambulia kwa
mapanga hadi kufa.Aliiambia mahakama hiyo kuwa mwaka 2005
watuhumiwa hao walikula njama za kumuua Mugisa ambaye ni mume wake na Catherine
John.
Alidai kuwa walifanya hivyo ili mjane
wa marehemu aolewe na Makomelo, huku Lutonja akilipwa sh. 20,000 ili amsaidie
kufanikisha mauaji hayo.Makandara aliomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali kwa washtakiwa hao ili
iwe fundisho kwa watu wanaojichukulia sheria mkononi
No comments:
Post a Comment