- RAIS KENYATTA ATANGAZA SIKU TATU ZA KUOMBOLEZA
- JESHI LA KENYA LAHITIMISHA KIBARUA KIGUMU
- AL SHABAAB WADAI MATEKA 137 WAMEUAWA,WAONYA
Waandishi Wetu n a Mashirika ya Kimataifa
Kenya imeanza siku tatu za
maombolezo ya kitaifa kwa waathirika wa mashambulizi ya kigaidi yaliyofanyika
katika jengo la kibiashara la Westgate mjini Nairobi na kusababisha mapigano yaliyodumu
kwa siku nne. Rais Uhuru Kenyatta amesema bendera zitapepea nusu mlingoti kuanzia jana kwa heshima ya waliopoteza maisha yao katika mashambulizi hayo. Katika hotuba yake kwa taifa juzi usiku, Rais Kenyatta alisema kuwa alihisi uchungu mkubwa na kuwa Kenya imejeruhiwa vibaya, lakini alielezea matumaini kwa kuwa shambulizi limeisha na kusema kwamba waliohusika watakiona cha mtemakuni.
Juzi Rais Kenyatta ametangaza kuwa operesheni za
kijeshi dhidi ya magaidi zimemalizika katika maduka ya kifahari ya Westgate.Alisema Kenya imewaaibisha washambuliaji
hao, kwa kuua magaidi watano na kuwakamata wengine 11 ambao wamezuiliwa. Katika tukio hilo
Watu 62 wameuawa ikiwemo wanajeshi watatu na wengine 8 wamejeruhiwa. Habari
kutoka Kenya
zinaeleza kuwa kuna hofu kuwa idadi ya watakaofariki huenda ikaongezeka.
Maafisa wa uchunguzi wa kimataifa wanaungana na wale
wa Kenya kujaribu kuondoa
miili ambayo imenaswa kwenye vifusi vya jengo hilo ambalo sehemu yake iliporomoka jana.Nia ni kujaribu pia kutambua uraia wa washambuliaji
hao. Baraza la usalama wa kitaifa lilitarajiwa kukutana
jana kudadisi yaliyotokea na kujiandaa kwa mkakati mpya wa kukabiliana na
magaidi.
Magaidi watatu wa kundi la Al Shabaab lililokiri
kutekeleza mashambulizi hayo,waliuawa katika shambulizi hilo lililodumu kwa
siku nne na kuwa washukiwa we n g i n e 11 wa l i k ama twa wakijaribu kuondoka
nchini.Wakati huo huo, ofisa
mmoja mkuu wa serikali ya Somalia,
amesema kuwa hakuna suluhu la kijeshi kwa kundi la wanamgambo wa Al Shabaab
nchini humo. Wanamgambo hao wamekiri kuhusika na mashambulizi ya kigaidi nchini
Kenya.
Akizungumza na mjumbe wa nchi hiyo katika Umoja wa
Mataifa, Yusuf Mohamed Ismail Bari Bari, alisema kuwa serikali yake na jamii ya
kimataifa inapaswa, kuangazia zaidi mizizi ya tatizo la magaidi hao,
upatikanaji wa rasilimali pamoja na uwakilishi wa kisiasa.Wakati huo huo, Wataalamu wa uchunguzi wa
Kisayansi kutoka nchini Ufaransa na Israel
wamewasili nchini Kenya
kushirikiana na wazawa ili kujua silaha zilizotumika wakati wa shambulizi hilo la kigaidi.
Wataalam hao wanalenga kubaini ni aina gani ya
milipuko ilitumika kulipulia jengo hilo.Pia maofisa wa Serikali bado wapo eneo la tukio ili
kuhakikisha usalama unakuwepo. Televisheni ya nchi hiyo ya Q TV imesema kuwa kazi
ambayo ilikuwa nimeanza ni ya kuondoa vifusi ili kuweza kuondoa maiti
zilizofukiwa baada ya sehemu ya jengo hilo
kuanguka.
Kwa mujibu wa matangazo hayo maiti hizo
zitatambuliwa kwa kutumia kipimo cha DNA. Matangazo ya televisheni hiyo
yalieleza kuwa ndani ya jengo hilo
la kibiashara moshi mkubwa ulikuwa ukizidi kufuka lakini hakukuwa na taarifa
zozote kwa waandishi wa habari kuhusu ni nini kilichokuwa kikiendelea.
Katika hatua nyingine, Serikali
ya Kenya
imetangaza donge nono la dola milioni 25 kwa mtu yeyote atakayefanikisha
kupatikana kwa magaidi sugu ulimwenguni. Tayari FBI imetoa orodha ya magaidi 23
wanaotafutwa.
Wakati huo huo, wanamgambo wa Al-Shabaab
kutoka Somalia jana walidai
mateka 137 waliokuwa wakiwashakilia waliuawa katika jumba la kibiashara la
Westgate jijini Nairobi.Kwa mujibu wa shirika la habari la Ufaransa, AFP,
idadi kamili ya waliokufa imekuwa ngumu kujulikana na inaweza ikawa ni kubwa
zaidi kuliko idadi ya walioorodheshwa kukosekana.
Wapiganaji hao wenye uhusiano na al-Qaeda, katika
ujumbe waliouweka kwenye mtandao wa Twitter, walisema "mateka 137
waliokuwa wakishikiliwa na mujahedeen" wamekufa."Wanamgambo hao pia waliwatuhumu
wanajeshi wa Kenya
kwa kupiga makombora yenye sumu kuhitimisha mapambano ya kuwasaka.
Matukio ya ubabe wa Al-Shabaab
Haya ni miongoni mwa mashambulizi makubwa
ya kigaidi ambayo yamewahi kutekelezwa katika Kanda ya Afrika Mashariki.
Taarifa zinazohusiana
na Kenya
Septemba 21, 2013: Magaidi
walitumia guruneti na bunduki kushambulia jengo la kifahari la Westgate mjini
Nairobi, Kenya lenye maduka na mikahawa 80 na kuwaua watu 62 huku zaidi ya 175
wakijeruhiwa.Kundi la kigaidi la Al-Shabaab lilikiri kufanya
shambulio hilo.
Oktoba 2011-Machi 2013: Al Shabaab
na wapiganaji wake walifanya mashambulizi kadhaa nchini Kenya na kuwaua zaidi ya watu sitini wakilipiza
kisasi kile walichosema ni hatua ya Kenya
kupeleka majeshi yake nchini huo kupigana dhidi yao.Serikali ya Kenya
ilituma vikosi vyake nchini Somalia
baada ya al-Shabaab kufanya mashambulizi kadhaa katika maeneo ya mipakani
pamoja na kuwateka nyara watalii wa kigeni.
Julai 11 , mwaka 2010 : Wanamgambo
wa Al Shabaab walilipua mabomu katika mji mkuu wa Uganda Kampala, katika
mkahawa ambako mashabiki wa soka walikuwa wanatazama fainali ya michuano ya
Kombe la Dunia, kwenye televisheni kubwa.
Takriban watu 76 waliuawa. Kundi la Al-Shabaab
lilisema kuwa mashambulizi hayo yalikuwa ya kulipiza kisasi kwa Uganda kujihusisha na vita dhidi ya kundi hilo Somalia.Novemba 28, mwaka 2002: Kundi hilo la kigaidi lilishambulia hoteli ya kifahari iliyokuwa
inamilikiwa na Waisraeli, katika eneo la Kikambala karibu na mji wa Mombasa na kuwaua watu
13.
Dakika chache kabla ya shambulizi hilo,
magaidi hao waliifyatulia makombora ndege ya Israel
iliyokuwa inaruka katika Uwanja wa Kimataifa wa Mombasa, lakini waliikosa.Agosti 7, mwaka 1998: Kundi
lingine la kigaidi la al-Qaeda lilishambulia balozi za Marekani mjini Nairobi na Dar es
Salaam. Mashambulizi hayo yaliwaua watu 224 , wengi
wakiwa Wakenya . Raia 123 wa Marekani pia waliuawa.
No comments:
Post a Comment