26 September 2013

MTIBWA SUGAR: SARE SASA BASI



 Na Fatuma Rashid
  Timu ya Mtibwa Sugar imedhamiria kuondoa mdudu wa sare anayeiandama timu hiyo mara kwa mara.Akizungumza kwa simu akiwa Morogoro Katibu Mkuu wa timu hiyo, Salum Kijazi alisema hivi sasa wanajipanga ili waweze kufanya vizuri katika mechi dhidi ya Ashanti United.

   Kijazi alisema katika mechi, lazima kunakuwa na upungufu mbalimbali ambao husababisha wapinzani kutumia kama faida, hivyo timu yake inaendelea kurekebisha makosa yaliyojitokeza.
"Unajua katika kila mechi kuna upungufu wake na mpinzani wako hutumia kama faida, ila kwa kipindi hiki timu imejipanga vizuri na imefuta makosa yote ambayo kama tusingeyarekebisha tungekuwa katika nafasi mbaya," alisema.
  Alisema msimu huu kila timu ipo vizuri, hivyo inasababisha kila mechi wawe wanajiandaa vizuri na kutumia kila mbinu katika mechi."Katika mpira unapoingia uwanjani hautakiwi kukurupuka, wachezaji wanatakiwa kujipanga na kujua ni mbinu gani wanazotumia timu pinzani, ili waweze kupambana nao, hivyo vijana wanajipanga ipasavyo kwani ligi inazidi kupamba moto kutokana na kila timu kujiandaa vizuri," alisema.
  Akizungumzia waamuzi wanaochezesha Ligi Kuu msimu huu, Kijazi alisema katika mechi iliyopita dhidi ya Prisons mwamuzi alikuwa akifanya makosa hivyo walichukulia kama makosa ya kawaida.
"Waamuzi wote wanachezesha vizuri, ila kuna makosa y a k i b i n a d amu amb a y o huwa yanatokea kwani huyo anayechezesha ni binadamu pia hivyo kuna haja ya kukaa na kuongea naye," alisema.
   Alisema katika mechi dhidi ya Ashanti wamejipanga kufanya vizuri, licha ya kuwa na majeruhi ambao ni Mussa Hassan 'Mgosi' na Masudi Ally, walioumia wakati wa mazoezi lakini wanaamini katika mechi hiyo wataweza kucheza kutokana na hali zao kuwa nzuri.

No comments:

Post a Comment