Na Yusuph
Mussa, Korogwe
MCHUNGAJI wa Kanisa
la Anglikana, Wilaya ya Korogwe, mkoani Tanga, Stephen Daffa, amesema Tanzania ya
sasa, ili wafanyakazi wasikilizwe na kupata haki zao, lazima wagome au
kuandamana; hivyo Tume ya Mabadiliko ya Katiba, ikubali kuingiza kipengele
hicho kwenye Katiba Mpya.Alisema
kipengele hicho kikiwepo, waajiri wataona umuhimu wa kusikiliza na kutatua kero
za wafanyakazi wao.
Mchungaji
Daffa aliyasema hayo mwishoni mwa wiki kwenye Kikao cha Maboresho ya Rasimu ya
Katiba Mpya kilichoandaliwa na Asasi ya Tanzania Environment Relatives
Organization (TERO) ya Mjini Korogwe kwa ufadhili wa Shirika la The Foundation
for Civil Society la Dar es Salaam.
Mkutano
huo ulishirikisha wananchi wa Kata za Kerenge na Magoma wilayani humo ambapo
akichangia maoni hayo, Bw. Ramadhan Mswaki, alisema badala ya mwalimu au daktari
kuchukua uamuzi wa kugoma kwa madai ya kuonewa au kupunjwa mshahara, waandike
barua ya kuacha kazi.
Naye Mwalimu Edith Kimea, aliomba Katiba Mpya iwe na
kipengele cha kutoa uhuru kwa viongozi wa wafanyakazi ili wasiendelee kutishwa
na viongozi wa Serikali unapotokea mgomo ambapo hivi karibuni, Katibu wa Chama
cha Walimu nchini (CWT), Wilaya ya Korogwe, Fesstus Mitimingi, alikuwa
anatafutwa ili awekwe ndani..
No comments:
Post a Comment