30 September 2013

KENYA YAINGIA VITANI


NAIROBI, Kenya

  Serikali ya Kenya, imesema nchi hiyo ipo katika vita na wapiganaji wa jihadi kutoka nchini Somalia Al Shabaab.Pia Serikali nchini humo imekanusha taarifa zinazodai k uwe p o kwa s h amb u l i o linalodaiwa kufanywa na Al Shabaab katika jengo la kibiashara la Westgate, Septemba 21 mwaka huu, zilipuuzwa
. Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), watu 67 walipoteza maisha katika shambulio hilo ambalo lilidumu kwa siku nne ndani ya jengo hilo.Juzi usiku, Wakenya na raia wa nchi nyingine waliopoteza ndugu zao katika shambulio hilo, waliwasha mishumaa nje ya jengo hilo ili kuwakumbuka waliokufa.   Magazeti ya Kenya yalidai Idara ya Usalama nchini humo ilitoa ilani mwaka mmoja uliopita juu ya watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa Al Shabaab, kupanga kufanya mashambulizi Mjini Nairobi na Mombasa.

    Inadaiwa watu hao walipanga kufanya mashambulizi ya kujitoa mhanga na kulishambulia jengo hilo.

Kamati ya Ulinzi ya Bunge nchini humo, inakutana leo kuliangalia suala hilo na ilani iliyotolewa. Ofisa mmoja mwandamizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani nchini humo, alisema Serikali imekuwa ikipata taarifa kama hizo kila siku.

   Aliongeza k uwa , hatua zimekuwa zikichukuliwa kuepusha mashambulio mengi ambapo Kenya iko vitani na kila siku kijana wa Kenya anashawishiwa na Al Shabaab kuua Wakenya.

No comments:

Post a Comment