Na Rose
Itono
Jeshu la Polisi Kanda Maalumu Dar es
Salam, limesema kuanzia leo benki zote zilizopo jijini humo zitalindwa na
askari wa jeshi hilo
ili kuzuia wimbi la matukio ya ujambazi katika benki.Kamanda wa
Polisi wa kanda hiyo, Kamishna Suleiman Kova, aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na
waandishi wa habari
. Alisema mtandao
huo, unahusisha baadhi ya watumishi wa benki hizo ambao si waaminifu ambapo
wahalifu hutumia sare za jeshi hilo
kufanikisha uhalifu wao.Aliongeza kuwa, hatua hiyo imelenga
kutimiza wajibu wa jeshi hilo
kuhakikisha matukio ya aina hii hayatajirudia na kuongeza kuwa, wasiokubaliana
na hatua hiyo wafunge benki zao.
Kamishna Kova alisema, jeshi hilo limebaini ujambazi
huo unafanyika kupitia mtandao wa wafanyakazi wa benki ambao wanashirikiana na
baadhi ya walinzi wa kampuni binafsi."Matukio haya yanaonesha wahalifu
wanakuwa na taarifa muhimu za benki husika pamoja na kujua
watunzaji funguo za chumba cha kuhifadhia fedha na kiasi ambacho kimeingia
benki.
"Kutokana na mazingira hayo, jeshi
letu likiwa na wajibu wa kulinda maisha ya watu na mali zao, tumechukua hatua
madhubuti na makusudi ili kukomesha wizi huo ambao unaendelea," alisema.
Alisema benki zote jijini humo
zitalazimika kufuata utaratibu uliowekwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT), ili kuhakikisha siri za benki
hazivuji kwa wahalifu kama ilivyo sasa. Aliongeza kuwa, matukio kama hayo ni tishio kwa wawekezaji nchini na kuwataka wamiliki wa banki, kutumia vifaa vya kisasa ili kuimarisha ulinzi ambavyo vitatunza kumbukumbu au kutoa tahadhari ya haraka kama kuna tishio la kiusalama.
Pia alizitaka benki hizo kuwa
waangalifu na ajira za wafanyakazi wao kabla ya kuwaajiri na kuwafanyia upekuzi
wa kina ambapo jeshi hilo
litatoa ushirikiano wa kuweka kumbukumbu za watumishi wao na kuwataka kuwatumia
kampuni binafsi za ulinzi zenye viwango vya kulinda na kusafirisha fedha zao.
Aliwataka wafanyakazi wa benki, kuvaa
sare, kupewa mafunzo ya kujihami kiusalama pamoja na mbinu mbalimbali za
kuwatambua wahalifu wanaojihusisha na wizi wa mtandao."Tunasisitiza matumizi ya
teknolojia ya kisasa kama kamera za CCTV,
mawsiliano ya moja kwa moja na vyombo vya dola kabla, wakati au baada ya tukio.
"Makamanda wote wanapaswa
kujipanga upya dhidi ya matukio kama haya,
majambazi wanaofanya matukio ya uhalifu, acheni mara moja kwani oparesheni ya
kuwasaka na kuwakamata itafanyika katika mikoa yote chini," alisema.
Kamishna Kova alisema, jeshi hilo linamshikilia mmoja
kati ya watu wanaojihusisha na matukio ya aina hiyo, Azim Chokera (47) mwenye
asili ya Kiasia ambaye ushahidi wa awali unaonesha amejihusisha na matukio
mawili ya wizi wa benki na amekiri kufahamu mwenendo wa tukio la wizi wa Benki
ya Habib.
No comments:
Post a Comment