19 September 2013

JK APIGILIA MSUMARI WANASIASA



Na Mwandishi Wetu
RAIS Jakaya Kikwete, ameshangazwa na kiwango cha uongo wa baadhi ya wanasiasa na hasa madai kwamba aliteua wajumbe wa Tume ya Katiba bila kuongozwa na mapendekezo ya wadau mbalimbali waliopendekeza majina hayo.

Aidha, Rais Kikwete amesema kuwa bado anaendelea kuamini kuwa mchakato wa Katiba Mpya utafikia mwisho wake mwakani, 2014, na hivyo kuiwezesha Tanzania kufanya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 chini ya Katiba Mpya.
Rais Kikwete aliyasema hayo Jumatatu, wiki hii, mjini San Rafael, California wakati alipokutana na kuzungumza na Jumuiya ya Watanzania waishio Jimbo la California, nchini Marekani, wakati alipoanza ziara yake ya siku mbili katika Jimbo hilo ikiwa ni sehemu ya ziara yake nchini Marekani.
Vilevile, Rais Kikwete alisema hana tatizo na watu wanaopinga sera za Serikali au hata kumpinga yeye binafsi bali tatizo lake ni wanasiasa na wanaharakati wanaochochea ghasia, fujo na uvunjifu wa amani.
"Watu wote niliowateua walipendekezwa na wadau mbali mbali zikiwamo taasisi za dini. Yule Mama Maria Kashonda alipendekezwa na Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), Mama Mwantumu Malale alipendekezwa na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA). Kila kundi ambalo lilipendekeza watu limepata mjumbe katika Tume hiyo wakiwemo walemavu ambao naambiwa nimewasahau," alisema Rais Kikwete na kuongeza:
"Hivi nyinyi wanasiasa wenzangu mkikosa hoja mnaongopa hata kwa vitu ambavyo viko wazi kabisa. Tulikubaliana kuwa Rais angefanya uteuzi wa wajumbe wa Tume baada ya kupokea mapendekezo ya wadau mbali mbali na katika mchakato ulioendeshwa kwa uwazi kabisa. "Hivyo, ndiyo ilivyofanyika. Sasa uongo wa nini? Kama hakuna hoja ni kwamba hakuna tu na wala uongo hautasaidia."
Kuhusu mjadala wa karibuni kuhusu kama Rais awe na madaraka ya kuteua wajumbe 166 wa nyongeza ili kuingia katika Bunge la Katiba kujadili Rasimu ya Katiba Mpya, Rais Kikwete amesema kuwa yeye hana tabu kama itabidi ateue basi atateua, lakini kama si lazima yeye hatafanya hivyo.
"Mimi sina taabu, wakisema niteue basi nitateua. Wakisema nisiteue vilevile sina taabu, isitoshe hiyo itakuwa inanipunguzia mzigo na kazi. Ile kazi yenyewe ya kuteua Wajumbe wa Tume ya Katiba ilikuwa siyo rahisi

No comments:

Post a Comment