Na
Mwandishi Wetu
Rais Jakaya Kikwete, amesema mwenendo
wa Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC), kuhusu Bara la Afrika na
viongozi wake, unainyima mahakama hiyo nafasi kubwa ya kuungwa mkono barani
Afrika
. Alisema
kuanzishwa kwa ICC kumetokana na Mkataba wa Rome ambao ulikuwa ni hatua muhimu katika
mfumo wa kimataifa kupambana na makosa ya jinai.Rais Kikwete
alitoa msimamo huo mwishoni mwa wiki wakati akilihutubia Kikao cha Baraza Kuu
la Umoja wa Mataifa (UNGA), katika Makao Makuu ya umoja huo, New York, Marekani.
Katika hotuba
yake, Rais Kikwete pia alilaani mashambulizi yanayoongezeka dhidi ya vikosi vya
kimataifa vya kulinda amani katika nchi mbalimbali duniani vikiwemo kutoka Tanzania."Kwa
hakika, kuundwa kwa mahakama hii kuliweka mfumo mzuri wa kuondokana na watu
kutenda vitendo vya jinai, hata hivyo mwongo mmoja baada ya kuanzishwa mahakama
hii, mvutano umezuka kati ya ICC na Bara la Afrika.
"Sasa
mahakama hii inaonekana kama taasisi isiyojali
maoni na msimamo wa Afrika kwa mambo ambayo kwa maoni yangu ni hofu halali ya
Waafrika," alisema Rais Kikwete.Aliongeza kuwa,
bado mahakama hiyo inaendelea kupuuza maombi ya mara kwa mara ya Umoja wa
Afrika, hivyo ni jambo la kutia huzuni kuwa maombi ya kubadilisha muda wa
kuanza kusikilizwa kwa kesi dhidi ya Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya; na Naibu
Rais William Ruto yalipuuzwa na hayakujibiwa.
"Tabia hii
imekuwa ni tatizo kubwa linaloleta kikwazo kwa ICC kushindwa kutimiza wajibu
wake wa kupambana na tabia ya watu wanaofanya makosa ya jinai kutokuchukuliwa
hatua."Kwa
hakika, kugangamara kwa ICC hata katika masuala yaliyo wazi, kumethibitika kuwa
kunainyima mahakama hii nafasi ya kuendelea kuungwa mkono Barani Afrika,"
alisema.
Rais alisema Tanzania ni moja ya nchi zinazoshiriki shughuli
za kimataifa za kulinda amani chini ya Umoja wa Mataifa ikiwa na zaidi ya
walinda amani 2,500 Darfur, nchini Sudan,
Lebanon
na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).
Alisema Tanzania ni
nchi ya sita katika Afrika na 12 duniani kwa kutoa walinzi wa amani duniani
ikiridhishwa na mchango mdogo wanaoutoa katika shughuli hiyo.Aliongeza kuwa,
wakati mwingine Tanzania
inalipa gharama kubwa na maisha ya vijana wake katika shughuli hizi kama
ilivyotokea Darfur na DRC ambapo askari wake
ambao ni walinda amani walipoteza maisha. Rais Kikwete
alikuwa katika ziara ya kikazi nchini Marekani na Canada na atarejea nchini leo.
No comments:
Post a Comment