18 September 2013

INUKA YAKOPESHA WAJASIRIAMALI 29,000



ZAIDI ya sh.milioni35 zimetumika kwa ajili ya kuwakopesha wajasiriamali wadogo na wakubwa kwa ajili ya kuendeleza biashara zao, anaripoti Re hemaM aigala.
Akizungumza katika mafunzo ya ujasiriamali juzi jijini Dar es Salaam,Ofisa Mikopo wa Taasisi ya Inuk a Wanawake na Maendeleo, David Msuya alisema tayari wameshakopesha pesa hizo kwa wajasiriamali wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Alisema kuwa,katika Mkoa wa Dar es Salaam tayari wanachama 29,000 ambao wengi wao wamesha kopeshwa mkopo mdogo ambao hauna riba unaoanzia sh. 30,000.
Hata hivyo, alisema hivi karibuni wamepata wajasiriamali wapya 30 wanaotoka Mbezi Mpigi Magoe, Wilaya ya Kinondoni ambapo tayari wameshawakopesha sh. milioni 1.8.
Vile vile, Msuya alisema hivi sasa wana vituo 16 ambavyo vipo Dar es Salaam, Shinyanga, Tanga, Tunduru, Lindi na Mtwara.Hata hivyo, ofisa mikopo huyo aliwataka wajasilimari kuwa wa kweli katika biashara zao na kuwa wabunifu.
“Mjasiriamali yeyote anatakiwa kuwa mbunifu wa kujua leo atengeneze nini ili aweze kupata wateja wengi kushinda mwenzake na si kuigizana bidhaa,” alisema Msuya.Hata hivyo, taasisi hiyo ilisema lengo lake ni kuinua wajasiriamali wa chini ili waweze kuwa wakubwa

No comments:

Post a Comment