07 September 2013

HATUWEZI KUTENGWA EAC-MEMBE



 Na Goodluck Hongo
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Bernard Membe, amesema kamwe Tanzania haiwezi kutengwa na nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC).Alisema Tanzania ina rasilimali za kutosha kama bandari, barabara nzuri, chakula cha kutosha ambazo ni vigumu kwa nchi hizo kuchukua uamuzi huo
.Bw. Membe aliyasema hayo Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana.Akizungumzia mkutano wa Viongozi wa Maziwa Makuu uliofanyika juzi nchini Uganda, Bw. Membe alisema wakuu hao wametia siku 17 kwa waasi wa M23 na Serikali ya Congo (DRC), kumaliza mgogoro wao.
Kama mgogoro huo hautapatiwa ufumbuzi ndani ya siku hizo, viongozi hao watakutana tena na kujadili hatua za kuchukua."Wa k u u w a n c h i h i z i wamekubaliana kutoa siku 17 kwa waasi wa M23 na Serikali ya DRC ili wamalize mgogoro wao, Rais wa Uganda, Yoweri Museveni ataendela kuwa msuluhishi wa mgogoro huo na nchi zote za Maziwa Makuu," alisema Bw. Membe.
Aliongeza kuwa, mazungumzo kati ya Rais Jakaya Kikwete na Rais wa Rwanda, Paul Kagame, yalifanyika kwa mafanikio makubwa na yalichukua zaidi ya saa moja kila mmoja akitoa la moyoni ambapo kinachotarajiwa kutokea kwa siku zijazo ni kuona mikutano ya viongozi wa nchi hizo inafanyika katika nchi ya Rwanda na Tanzania ili kuimarisha uhusiano.
Bw. Membe alisema, kuhusu mgogoro wa Tanzania na Malawi kuhusu Ziwa Nyasa, alisema hadi sasa kuna jopo la wataalamu wa sheria nchini, lipo nchini humo wakifanya mazungumzo.
Akizungumzia Uchaguzi Mkuu nchini Madagascar unaotarajiwa kufanyika Oktoba mosi mwaka huu, kutakuwa na wagombea 33 wa nafasi ya urais na kama mshindi hatapatikana kutokana na wingi wa wagombea hao, utarudiwa tena Oktoba 20,2013.

No comments:

Post a Comment