10 September 2013

EXIM YATUNISHA MFUKO WA NYERERE



 Na Mwandishi Wetu
BENKI ya Eximim ekabidhi shilingimilion i10, kwaBenkiKuuyaTanz ania(BoT) zitaka zot um ikakus aidiaMfukowaUdha mini waBen kiKuumaaruf u k ama'Mwali muJu lius Nyere reMemorial Schol arshipFund'iki wa ni dhamira yaBenki yaEximku ungam konojit ihadaza ku endele zasekta ya elim unchin i
.Benk iKuumapem amwezi uliopitail itanga za kuwaita dhaminiwanaf unzi s itawae limu yajuuwaliokatikakiw ang ochas hah ada yakwanzana shahada ya uzamiliwa naosome am asomoyahesabu, sayans i nateknolojia chini ya mfukohuo.
Akizung umzaw aka tiwah aflaya kukabidhimsaada huoDa r es Salaa mmwishoni mwa wiki ,Kaimu Gavana wa BoT, Sera za Uchumi na Fedha Dkt. Natu Mwamba,alisema mfuko huo umejikita katika kudhamini wanafunzi wa kike katika shahada ya kwanza wanaosoma hesabu, sayansi na teknolojia katika vyuo vikuu nchini mwaka huu.
"Fedha zitakazopatikana katika mfuko huu zitatumika kudhamini wanafunzi wote wa kike na kiume wa Tanzania wanaosoma shahada ya kwanza katika masuala ya uchumi, tehama, heasabu na fedha pamoja na wanafunzi wanaolenga kusoma shahada ya uzamili katika maeneo hayo.
"Udhamini utatolewa kwa kufuata sifa za kitaaluma na kupitia mchakato mkali wa uteuzi wa wadhaminiwa, alisema na kuongeza kwamba waombaji watakaofanikiwa watapata udhamini kamili pamoja na kupewa laptop," alisema.
Dkt. Mwamba alisema kuwa udhamini huo utalenga gharama za moja kwa moja za chuo ikiwa ni ada na usajili na pamoja na gharama nyingine za mwanafunzi zikiwemo chakula, malazi, vitabu na vifaa vya kujisomea isipokuwa gharama za mafunzo kwa vitendo, mahitaji maalum ya masomo na gharama nyingine kama zilivyoorodheshwa na chuo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Exim, Bw. Anthony Grant alisema benki hiyo inatambua umuhimu wa kusaidia elimu kwa maendeleo ya vijana kwa kuwa wao ndo viongozi wa baadaye wa Taifa hili.
Naye Meneja Masoko Msaidizi wa Benki ya Exim, Bi Anita Goshashy, aliongeza kuwa benki yake imekuwa mstari wa mbele kusaidia jitihada mbalimbali za kusaidia maendeleo ya jamii zikiwemo afya na elimu.
Mfuko wa Udhamini wa Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere ulizinduliwa jijini Arusha mwaka jana na Rais Jakaya Kikwete ukiwa na lengo la kukuza elimu katika masomo ya hesabu, sayansi na teknolojia kwa wanafunzi wa kike.
Kila mwaka mfuko unalenga kudhamini takriban wanafunzi 25 wenye vigezo na wanaofaidika na udhamini ni pamoja na wanafunzi wa kike waliofaulu zaidi katika masomo ya hesabu na sayansi.  

No comments:

Post a Comment