09 September 2013

ALBINO KUFANYIWA UKAGUZI WA AFYA



CHAMA cha walemavu wa ngozi (Albino) nchini kwa kushirikiana na madaktari kutoka Hospitali ya Taifa ya Rufaa ya Muhimbili wanatarajia kufanya ukaguzi wa afya kwa jamii ya walemavu wa ngozi mkoani Tanga katika wilaya tatu za Muheza, Lushoto na Korogwe.Kazi hiyo inatarajiwa kufanyika kuanzia Septemba 22,23 na 24 mwaka huu katika wilaya hizo
. Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho, Ernest Kimaya alisema hayo wakati wa kikao cha kujadili changamoto zinazowakabili jamii hiyo katika upatikanaji wa huduma za afya kilichowahusisha wadau wa sekta ya afya elimu na huduma nyingine muhimu za kijamii mkoani Tanga.
Kimaya alisema kazi hiyo ambayo wanaamini itawasaidia walemavu wa ngozi kutambua hali ya afya zao haitakuwa endelevu kutokana na ufinyu wa bajeti. "Tungetamani sana kampeni hii iwe endelevu lakini kutokana na ufinyu wa bajeti itabidi ifanyike katika wilaya chache tu ila tunaomba wafadhili waendelee kujitokeza ili tufikie watu wengi zaidi," alisema Mwenyekiti huyo.
Hata hivyo kutokana na hali hiyo aliiomba Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kuanzisha kliniki za matibabu ya ngozi katika hospitali na vituo vya afya nchini kwa ajili ukaguzi wa afya walemavu wa ngozi ili walioathirika na ugonjwa wa saratani ya ngozi waweze kujitambua mapema. "Unajua tukienda hospitalini watu wanaishia kupewa dawa za kuzuia mionzi ya jua tu lakini kumbe mwingine tayari ameathirika na saratani tunaomba kuwe na utaratibu maalum kwa ajili ya walemavu wa ngozi katika vituo vyote vya afya na hospitali za hapa nchini," alisisitiza Kimaya.
Kuhusu changamoto za ukosefu wa huduma muhimu zinazokosekana kwa walemavu wa ngozi, Ofisa Ustawi wa Jamii Sekretarieti ya Mkoa wa Tanga, Eveline Hijja ameziagiza taasisi za afya za Serikali kuwapa kipaumbele walemavu wa ngozi mara wanapofika katika hospitali na vituo vya afya ili kuepuka dhana ya unyanyapaa iliyojengeka miongoni mwa jami

No comments:

Post a Comment