09 September 2013

AIRTEL YAPONGEZWA KUPUNGUZA AJALI



Na Mwandishi Wetu
KA M P U N I y a mitandao ya simu za mkononi nchini, Airtel imetajwa kuwa moja kati ya kampuni ambazo zimekuwa zishirikiana na Serikali kwa dhati katika harakati za kupambana na tatizo la ajali za barabarani.Kauli hiyo ilitolewa na Kamanda wa Kikosi cha Us alama Barabarani, Mohamed Mpinga, wakati akieleza juhudi ambazo zimekuwa zikichukuliwa na kampuni hiyo.

Alisema Airtel imeweza kutoa mchango mkubwa wa kupunguza wimbi la ajali za barabarani kwa kiasi kikubwa."Airtel ni wadau wakubwa wa kampeni za usalama barabarani, kwa miaka mitano mfululizo na hata mwaka huu 2013 Airtel inaendelea na udhamini wa wiki ya nenda kwa usalama barabarani.
"Airtel pia imedhamini vipindi vya elimu ya usalama barabarani katika televisheni na redio, pia Airtel kwa kushirikiana na Rotary club na Jeshi la Polisi usalama barabarani imedhamini kampeni yenye ujumbe usemao Kuendesha + Simu = Kifo inayowaonya waendesha vyombo vya moto kutotumia simu wakati wakiendesha magari," alisema Mpinga.
Alisema mwaka jana Airtel ilidhamini mashindano ya mpira wa miguu kwa wapanda pikipiki (bodaboda) yaliyokuwa na lengo la kutoa elimu ya usalama barabarani kwa waendesha pikipiki.Naye Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel- Tanzania, Beatrice Singano Mallya, akizungumza juu ya suala hilo alisema "Airtel imeamua kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha inatokomeza kabisa wimbi la ajali za barabarani.
Alisema idadi ya vifo vinavyotokea barabarani ni kubwa mno na ndiyo maana Airtel imeamua kujikita katika kuokoa maisha ya wateja wake na Watanzania kwa ujuma.Alisema Airtel itaendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi usalama barabarani kuhakikisha lengo la kupunguza ajali linafanikiwa.

No comments:

Post a Comment