06 September 2013

AIRTEL YATOSHA YATANGAZA MSHINDI WA PILI WA NYUMBA



Na Frank Monyo
KAMPUNI ya simu za mkononi ya Airtel imemtangaza ofisa wa Benki Kuu, Bi. Anna Lyimo (29), mkazi wa Dar es Salaam kuwa mshindi wa pili wa nyumba aliyepatikana kupitia promosheni maalumu inayofahamika kwa jina la Airtel Yatosha shinda nyumba
.Akizungumza baada ya kuchezeshwa kwa droo hiyo jana Dar es Salaam, Meneja Uhusiano wa Airtel,Bw.Jackson Mmbando alisema Airtel inayo furaha kuchezesha droo ya pili ya nyumba ambapo mshindi atapata nyumba ya kisasa ya vyumba vitatu, iliyojengwa na Shirika la National Housing iliyoko Kibada, Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Alisema kuwa Bi.Lyimo amejishindia nyumba yenye thamani ya sh. milioni 65 na kuwa mshindi wa pili kushinda nyumba baada ya Bw. Silvanus Juma kuibuka mshindi wa kwanza mwezi uliopita.Alisema kuwa mpaka sasa Airtel imetoa nyumba 2 kwa Watanzania huku washindi wengine 56 wakiondoka na sh. milioni moja kila mmoja.Aliendelea kwa kusema bado wateja wa Airtel w a n a w e z a k u e n d e l e a kushindania nyumba moja iliyobaki kwa kujiunga na vifurushi mbalimbali vya Airtel na mwisho wa siku mtu anaweza kuibuka mshindi wa nyumba au kushinda milioni moja kila siku.
Ili kushinda mteja anahitaji kupiga *149*99# na kuchagua kifurushi cha siku, wiki au mwezi baada ya hapo mteja atakuwa ameingia moja kwa moja katika promosheni ya Airtel yatosha shinda nyumba 3, itakayomwezesha kujishindia milioni moja kwa kila siku au nyumba kwa kila mwisho wa mwezi.Akielezea furaha yake mshindi huyo wa nyumba B i . L y i m o a l i s e m a : "Ninamshukuru Mungu kwa bahati hii na noamba Airtel waendelee kuleta mabadiliko kwa wateja wengine kama walivyofanya kwangu... nimekuwa nikijiunga na vifurushi vya Airtel Yatosha k a m a h u d u m a l a k i n i sikuwahi kudhani kama nitaweza kushinda, leo nimeamini kuwa promosheni hizi zinamlenga mtu yeyote na unaweza kuabahatika kushinda zawadi kubwa kama hiiĆ®
Airtel yatosha promotion bado inaendelea, nyumba mbili zenye thamani ya sh. milioni 65 kila moja zimeshazawadiwa kwa wateja na bado nyumba moja ambayo itatolewa mwezi wa kumi na zawadi ya pesa taslimu kiasi cha sh. milioni 34 ambazo bado hazijakabidhiwa.Airtel jana imezindua ofa mpya ya kifurushi cha siku cha Airtel Yatosha BABA LAO kinachomwezesha mteja kuwasiliana na mtandao wowote nchini kwa sh.499 mteja anapata dakika 20 za muda wa maongezi,sms 300 na internet MB 125, hii ni ya kwanza na pekee sokoni kutoka Airtel.

No comments:

Post a Comment