Na Gladness Mboma
BARAZA la
Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA CCC) limewaasa
watumiaji wa huduma za nishati na maji kuzingatia taratibu zilizoainishwa
katika kanuni inayohusu muda wa kikomo wa kuwasilisha malalamiko ili kusaidia
haki kutendeka wakati wa mchakato wa kushughulikia malalamiko husika.
Kwa mujibu wa
taarifa iliyotolewa jana Dar es Salaam kwa vyombo vya habari na Mwenyekiti wa
EWURA CCC Mhandisi Profesa Jamidu Katima alisema jana Dar es Salaam kuwa wanalo
jukumu la kisheria la kupokea na kusambaza taarifa zinazowahusu watumiaji wa
huduma za nishati na maji.
“Mamlaka ya
Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kupitia Tangazo la Serikali namba
10, ilichapisha kanuni na taratibu zitakazokuwa zikitumiwa na EWURA katika
kushughulikia malalamiko ya watumiaji wa huduma za nishati na maji.
“Kwa kuzingatia
jukumu hilo, Baraza linawaasa watumiaji wa huduma za nishati na maji kuzingatia
taratibu zilizoainishwa katika kanuni hizo, hususan kanuni inayohusu muda
kikomo wa kuwasilisha malalamiko EWURA, kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia haki
kutendeka wakati wa mchakato wa kushughulikia malalamiko husika,” alisema.
Alisema kwenye
kanuni ya muda kikomo, kanuni zimeainisha aina sita za malalamiko na kwamba
ukiukwaji wa muda kikomo uliowekwa unamaanisha kuwa mlalamikaji atakuwa
amepoteza haki yake ya kusikilizwa.
Prof. Katima alisema malalamiko hayo ni
pamoja na malalamiko yanayohusiana na kukatiwa huduma bila kufuata utaratibu
kupatiwa ankara zisizo sahihi, kushindwa ama kukataliwa kuunganishwa kwenye
huduma, kuuza ama kusambaza bidhaa za petroli zisizo na kiwango,kukiuka bei
elekezi zilizotolewa na EWURA kwa kuuza ama kusambaza bidhaa za petroli bila
kufuata bei iliyoainishwa na EWURA na huduma isiyokidhi kiwango.
“ Wa k a t i m a l a l a m i k o
yanayohusiana na kukatiwa huduma bila kufuata utaratibu, kupatiwa ankara zisizo
sahihi na kushindwa ama kukataliwa kuunganishwa kwenye huduma yamewekewa muda
kikomo wa miezi kumi na mbili kuwasilishwa EWURA, malalamiko ambayo yanahusisha
kuuza ama kusambaza bidhaa za petroli zisizo na kiwango yatatakiwa kuwasilishwa
EWURA ndani ya siku saba,” alisema.
Alisema muda wa kikomo wa kuwasilisha
malalamiko yote yanayohusu uuzaji ama usambazaji wa bidhaa za petroli bila
kuzingatia bei elekezi ni miezi sita, wakati muda kikomo wa malalamiko yote
yanayohusisha huduma mbovu ni miezi ishirini na minne.
Wakati huo huo, alisema muda kikomo wa kuwasilisha
malalamiko ambayo hayapo katika makundi yaliyotajwa hapo juu ni miezi kumi na
mbili.
Alisema sababu hasa ya kutoa muda kikomo
wa kuwasilisha malalamiko ni kuongeza ufanisi katika kushughulikia matatizo y a
w a t u m i a j i wa huduma zinazodhibitiwa na EWURA kwa kuiwezesha kupata
ushahidi utakaoiwezesha kufikia uamuzi wa haki.
“Hivyo basi ni wajibu wa kila mtumiaji wa
huduma za nishati na maji kuzingatia kanuni na taratibu zote zilizowekwa kwenye
taratibu za kushughulikia matatizo ya watumiaji ili kuwezesha haki itendeke,”
alisema.
Al i s ema EWURA C C C lilianzishwa
chini ya sheria ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji ya mwaka 2001 ibara ya
414 kifungu cha 30 kwa lengo la kutetea na kulinda maslahi ya watumiaji wa
huduma za nishati na maji.
).
No comments:
Post a Comment